MAHAKAMA ya Rufani ya Tanzania muda mfupi uliopita imefuta rufaa dhidi ya Bilago Kasuku, Mbunge wa Jimbo la Buyungu (Chadema), anaandika Mwandishi Wetu.
Rufaa hiyo ilifunguliwa na aliyekuwa Mbunge wa jimbo hilo, Christopher Chiza, baada ya kumshinda katika Mahakama Kuu mwaka jana.
Kwa ushindi huo wa leo imebaki sasa rufaa yetu dhidi ya uamuzi wa Mahakama Kuu kumvua ubunge Mbunge wa Longido, Onesmo ole Nangole. Rufaa yake itasikilizwa Agosti 14, mwaka huu.
Leave a comment