Friday , 19 April 2024
Home Kitengo Maisha Afya Chadema wataka chanjo Covid-19 itolewe kwa lazima
Afya

Chadema wataka chanjo Covid-19 itolewe kwa lazima

Spread the love

 

CHAMA cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), kimeomba huduma ya utoaji chanjo ya ugonjwa wa homa kali ya mapafu, inayosababishwa na Virusi vya Corona (Covid-19), iwe ya lazima badala ya hiari kama ilivyotangazwa na Serikali. Anaripoti Mwandishi Wetu, Mwanza … (endelea).

Wito huo umetolewa leo Jumatatu, tarehe 19 Julai 2021 na Mwenyekiti wa Chadema Taifa, Freeman Mbowe, akizungumza na wanahabari jijini Mwanza.

“Serikali ya Rais Samia Suluhu Hassan, iweke utaratibu mzuri wa chanjo kuwa ya lazima kwa Watanzania,” amesema Mbowe.

Aidha, Mbowe ameitaka Serikali iongeze juhudi katika kutoa elimu kwa wananchi juu ya kujikinga na maambukizi ya Covid-19, kwa kuwa wengi hawachukui tahadhari dhidi ya janga hilo.

“Lakini public awareness (uelewa kwa umma) haiko, wala usifikiri Watanzania hawana akili, wamedanganywa hawajui washike la rais au la nani,” amesema Mbowe.

Freeman Mbowe, Mwenyekiti wa Chadema

Mbowe ameongeza “ wameweka usugu hawaogopi Corona, wanafikiri ugonjwa huu wanaambukiza wachache.”

Wakati huo huo, Mbowe ameiomba Serikali iweke mkakati wa kutoa matibabu ya Covid-19 bure kwa wananchi, kwa kuwa wengi hawana uwezo wa kumudu gharama za matibabu.

“Kitu kikubwa hatujakijua ni gharama za matibabu, kimsingi gharama za Covid-19 ilipaswa kusimamiwa na Serikali kwa asilimia 100,” amesema Mbowe na kuongeza:

“Sababu janga limetengazwa la kidunia na Shirika la Afya Duniani (WHO). Serikali na nchi zake zinawajibika kuwatibu na kuwakinga wananchi.”

Serikali ya Tanzania, imesema imekamilisha muongozo wa kuingiza na kutoa chanjo ya Covid-19, na kwamba zitaingizwa nchini hivi karibuni.

Katibu Mkuu wa Wizara ya Afya, Prof. Abel Makubi, alisema chanjo hiyo itatolewa bure kwa wananchi watakaohitaji.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

AfyaHabari za Siasa

Serikali yasaka watumishi afya ngazi ya jamii 8,900

Spread the loveSERIKALI imeanza utekelezaji wa mpango jumuishi wa wahudumu wa afya...

AfyaHabari za SiasaTangulizi

Bima ya afya kwa wote kuanza Aprili, wajane kicheko

Spread the loveSHERIA ya Bima ya Afya kwa Wote, inatarajiwa kuanza kutumika...

AfyaHabari Mchanganyiko

Marekani kuipa Tanzania bilioni 980 kudhibiti VVU, UKIMWI

Spread the loveSERIKALI ya Tanzania inatarajiwa kupewa msaada wa fedha kiasi cha...

AfyaHabari Mchanganyiko

Wanavijiji wajenga zahanati kukwepa umbali mrefu kupata huduma

Spread the loveWANAVIJIJI wa Kata ya  Musanja Jimbo la Musoma Vijijini, mkoani...

error: Content is protected !!