Thursday , 30 March 2023
Home Gazeti Habari za Siasa Chadema wabuni njia mpya kumkabili Rais Magufuli
Habari za Siasa

Chadema wabuni njia mpya kumkabili Rais Magufuli

John Mnyika, Mbunge wa Kibamba(wakwanza) na Boniface Jacob, Meya wa Ubungo
Spread the love

JOHN Mnyika, Naibu katibu mkuu wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) ambaye pia ni mbunge wa jimbo la Kibamba amesema kuwa rais Magufuli anatumia kivuli cha kuleta maendeleo kuminya demokrasia nchini, anaandika Hellen Sisya.

Akizungumza katika mkutano wa hadhara uliofanyika katika eneo la Kimara Mwisho jimboni humo,mbunge huyo amesisitiza kuwa demokrasia na maendeleo ni lazima viende pamoja.

“Rais Magufuli anataka kwa kivuli cha kuleta maendeleo, serikali isikosolewe pale inapokosea kuhusu maendeleo, kwa kuminya demokrasia, na sisi tunasema demokrasia na maendeleo ni lazima viende pamoja” alisema mbunge huyo.

Aidha, Mnyika aliongeza kuwa chama chake kitatumia mikutano ya kiserikali inayofanywa na wabunge pamoja na madiwani wake kufanya shughuli za chama kama ambavyo Rais Magufuli anatumia mikutano ya kiserikali kushughulika na kazi za chama chake.

“Kwa sababu rais Magufuli ameingia madarakani, amekataza mikutano ya vyama. Na anatumia mikutano ya kiserikali kushughulika na mambo ya CCM. Na sisi pia tumefikia uamuzi kwamba katika mikutano yetu yote ya hadhara, tutashughulika na masuala ya maendeleo, lakini pia tutashughulika na masuala ya demokrasia ” ,alisisitiza Mnyika.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

TEMESA iliyokarabati Kivuko kwa Bil 7.5 yapata hati chafu

Spread the love  MDHIBITI na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG),...

Habari za Siasa

ACT-Wazalendo yakusanya Mil 8.5/- kodi ya zuio na kutokomea nazo

Spread the love  MDHIBITI na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG),...

Habari za Siasa

DC Kasilda Mgeni ahamasisha chakula shuleni

Spread the love  MKUU wa Wilaya ya Same, mkoani Kilimanjaro, Kasilda Mgeni...

Habari za Siasa

Bilioni 223.9 zapelekwa Tunduru ndani ya miaka 2 ya SSH

Spread the love  ZAIDI ya Sh. bilioni 223.9 zimepelekwa Wilaya ya Tunduru...

error: Content is protected !!