Wednesday , 24 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Chadema wabuni njia mpya kumkabili Rais Magufuli
Habari za Siasa

Chadema wabuni njia mpya kumkabili Rais Magufuli

John Mnyika, Mbunge wa Kibamba(wakwanza) na Boniface Jacob, Meya wa Ubungo
Spread the love

JOHN Mnyika, Naibu katibu mkuu wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) ambaye pia ni mbunge wa jimbo la Kibamba amesema kuwa rais Magufuli anatumia kivuli cha kuleta maendeleo kuminya demokrasia nchini, anaandika Hellen Sisya.

Akizungumza katika mkutano wa hadhara uliofanyika katika eneo la Kimara Mwisho jimboni humo,mbunge huyo amesisitiza kuwa demokrasia na maendeleo ni lazima viende pamoja.

“Rais Magufuli anataka kwa kivuli cha kuleta maendeleo, serikali isikosolewe pale inapokosea kuhusu maendeleo, kwa kuminya demokrasia, na sisi tunasema demokrasia na maendeleo ni lazima viende pamoja” alisema mbunge huyo.

Aidha, Mnyika aliongeza kuwa chama chake kitatumia mikutano ya kiserikali inayofanywa na wabunge pamoja na madiwani wake kufanya shughuli za chama kama ambavyo Rais Magufuli anatumia mikutano ya kiserikali kushughulika na kazi za chama chake.

“Kwa sababu rais Magufuli ameingia madarakani, amekataza mikutano ya vyama. Na anatumia mikutano ya kiserikali kushughulika na mambo ya CCM. Na sisi pia tumefikia uamuzi kwamba katika mikutano yetu yote ya hadhara, tutashughulika na masuala ya maendeleo, lakini pia tutashughulika na masuala ya demokrasia ” ,alisisitiza Mnyika.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaTangulizi

Biteko ataja vipaumbele 7 bajeti nishati 2024/25

Spread the love  NAIBU Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Dk. Doto...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Mwekezaji amwaga bil. 39 kujenga viwanda 3 vya uchenjuaji

Spread the loveKampuni ya Mineral Access System Limited (MAST) inayoiwakilishwa kampuni ya...

Habari za SiasaTangulizi

Mpwa wa Magufuli mbaroni kwa kusambaza picha za utupu

Spread the loveJESHI la Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam limewakamata...

Habari za Siasa

Serikali kuanzisha mradi wa Gridi ya maji ya Taifa

Spread the loveWaziri wa Maji, Jumaa Aweso amesema katika mwaka wa fedha...

error: Content is protected !!