Friday , 29 March 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Chadema kuzindua mikutano ya hadhara kitaifa Januari 21
Habari za SiasaTangulizi

Chadema kuzindua mikutano ya hadhara kitaifa Januari 21

John Mrema, Mkurugenzi wa Itifaki, Mawasiliano na Mambo ya Nje Chadema
Spread the love

 

CHAMA cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), kitazindua rasmi mikutano ya hadhara kitaifa tarehe 21 Januari 2023, ikifuatiwa na uzinduzi wa mikutano hiyo katika ngazi ya Kanda nchi nzima. Anaripoti Mwandishi Wetu, Dar es Salaam … (endelea).

Taarifa hiyo imetolewa leo Ijumaa na Mkurugenzi wa Mawasiliano, Itifaki na Mambo ya Nje Chadema, John Mrema, akitoa maazimio ya Kamati Kuu ya chama hicho, iliyoketi jana tarehe 5 Januari 2023, kupokea na kujadili taarifa ya mwenendo wa mazungumzo ya maridhiano baina yake na Serikali ya Chama Cha Mapinduzi (CCM).

“Kamati Kuu imetangaza kuwa uzinduzi rasmi wa mikutano ya hadhara kitaifa utafanyika tarehe 21 January 2023 na utafuatiwa na uzinduzi wa mikutano ya hadhara kila makao makuu ya Kanda na baadae ngazi nyingine za chama zitaendelea na mikutano kwenye ngazi zao,” imesema taarifa ya Mrema.

Katika hatua nyingine, Mrema amesema kamati hiyo imeagiza ngazi zote za Chadema kuendelea na maandalizi ya mikutano ya hadhara.

Aidha, Mrema amesema kamati hiyo imeridhishwa na mwenendo wa mazungumzo ya maridhiano.

“Kamati Kuu imeridhishwa na mwenendo wa mazungumzo ya maridhiano baina ya timu ya Chadema inayoongozwa na Mwenyekiti wa Chama, Freeman Mbowe na ile ya CCM/Serikali inayoongozwa na makamu mwenyekiti wa CCM Bara, Abdulrahman Kinana,” imesema taarifa ya Mrema.

Kamati Kuu ya Chadema imetoa maazimio hayo baada ya Rais Samia Suluhu Hassan, kuondoa zuio la mikutano ya hadhara, lililodumu Kwa takribani miaka sita tangu 2016.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

Chadema yamtaka Rais Samia aunde tume kuchunguza mauaji mgodi wa Barick

Spread the loveRAIS Dk. Samia Suluhu Hassan, ameombwa aunde tume huru kwa...

KimataifaTangulizi

Zuma akataliwa kugombea urais

Spread the love  TUME Huru ya Uchaguzi Afrika Kusini (IEC) imemwondoa rais...

Habari za SiasaMakala & Uchambuzi

Nani anasema kuna hasara ATCL?

Spread the loveRIPOTI za makusanyo na matumizi ya fedha katika Kampuni ya...

Habari za SiasaTangulizi

CAG: Wastaafu, wenza wao chanzo NHIF kufilisika

Spread the loveRIPOTI ya ukaguzi ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu...

error: Content is protected !!