Thursday , 28 March 2024
Home Gazeti Habari za Siasa CCM yamtoa wasiwasi Rais Samia kuhusu mikutano ya hadhara
Habari za Siasa

CCM yamtoa wasiwasi Rais Samia kuhusu mikutano ya hadhara

Katibu Mkuu wa CCM, Daniel Chongolo
Spread the love

 

CHAMA Cha Mapinduzi (CCM), kimetoa wasiwasi Rais Samia Suluhu Hassan, kuhusu mikutano ya hadhara kwa kusema kuwa itatumia fursa hiyo kuwaeleza wananchi mazuri yaliyofanywa na Serikali yake. Anaripoti Mwandishi Wetu, Zanzibar … (endelea).

Hayo yamesemwa leo Jumanne, tarehe 10 Januari 2023 na Katibu Mkuu wa CCM, Daniel Chongolo, akizungumza katika hafla ya kufunga matembezi ya Umoja wa Vijana wa chama hicho (UVCCM), Visiwani Zanzibar, ambapo mgeni rasmi alikuwa Rais Samia.

Katibu Mkuu huyo wa CCM amempongeza Rais Samia kwa uamuzi wake wa kuondoa zuio la mikutano hiyo akisema itakisaidia chama chake.

“CCM kimefurahishwa sana na uamuzi wako wa kuruhusu mikutano ya hadhara kwa vyama, kwetu sisi CCM hiyo ni fursa muhimu na kubwa kwani tunakwenda kuitumia kueleza umma kile ambacho Serikali zetu zinafanya katika kutekeleza ilani ya chama. Nikuhakikishie hiyo fursa usiwe na wasiwasi nayo tuko makamanda wako,” amesema Chongolo na kuongeza:

“Tuko wasaidizi wako ambao tuko tyimamu tunakuhakikishia tutaitumia ipasavyo kuhakikisha tunapeleka kwa umma kile ambacho tunakifanya kupitia serikali zetu.”

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaMakala & Uchambuzi

Nani anasema kuna hasara ATCL?

Spread the loveRIPOTI za makusanyo na matumizi ya fedha katika Kampuni ya...

Habari za SiasaTangulizi

CAG: Wastaafu, wenza wao chanzo NHIF kufilisika

Spread the loveRIPOTI ya ukaguzi ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu...

Habari za SiasaTangulizi

Vikundi hewa 851 vyalamba bilioni 2.6 mikopo ya halmashauri

Spread the loveVIKUNDI hewa vya wajasirimali wadogo 851 kutoka katika halmashauri 19...

Habari za SiasaTangulizi

Mashirika matano yapata hasara mabilioni ya fedha

Spread the loveMASHIRIKA matano ya Serikali yanayojiendesha kibiashara, yamepata hasara ya mabilioni...

error: Content is protected !!