Thursday , 28 March 2024
Home Gazeti Habari za Siasa CCM yambomoa Zitto Kabwe Morogoro
Habari za Siasa

CCM yambomoa Zitto Kabwe Morogoro

Zitto Kabwe, Kiongozi wa ACT
Spread the love

WANACHAMA watatu wa Chama cha ACT -Wazalendo akiwemo aliyekuwa mgombea ubunge wa jimbo la Morogoro kusini Mashariki mwaka 2015 na Mwenyekiti wa jimbo la Morogoro  Kusini Mashariki wamehamia Chama Cha Mapinduzi (CCM),  anaandika  Christina Haule.

Wanachama hao yumo aliyekuwa mgombea nafasi ya ubunge katika uchaguzi mkuu uliopita Dk. Daud Mollel, Mwenyekiti wa chama hicho Dk. Hamimu Hongo na Yahya Nasoro mwanachama wa kawaida ambao wameamua kujiunga na CCM.

Wanachama hao wamesema kwa sasa hawana sababu ya  kuendelea kubaki upinzani kutokana na utendaji wa serikali ya awamu ya tano chini ya  Rais Magufuli.

Chama hicho ambacho kimepata pigo kinaoongozwa na Mwenyekiti wake,  Zitto Kabwe ambaye pia ni mbunge wa Kigoma mjini.

Makada  hao wapya wa CCM walijitokeza katika kikao cha Halmashauri Kuu ya mkoani morogoro na kuweka  bayana dhamira yao ya kuhamia CCM  na namna walivyoguswa na utendaji wa serikali ya awamu ya tano.

Katibu wa CCM mkoa wa Morogoro,  Kulwa Milonge ameitaka jamii  kuendelea kuwa na imani na serikali pamoja na kuendeleza ushirikiano katika kutekeleza Ilani ya chama ambayo ndiyo mwongozo kwa serikali.

Naye Mwenyekiti wa CCM wilaya ya Morogoro, Fikiri Juma amewataka wanasiasa hususani wa vyama vya upinzani kuangalia namna ya kushirikiana na serikali katika kupigania rasilimali za nchi na kuachana na siasa zisizo zingatia uzalendo.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaMakala & Uchambuzi

Nani anasema kuna hasara ATCL?

Spread the loveRIPOTI za makusanyo na matumizi ya fedha katika Kampuni ya...

Habari za SiasaTangulizi

CAG: Wastaafu, wenza wao chanzo NHIF kufilisika

Spread the loveRIPOTI ya ukaguzi ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu...

Habari za SiasaTangulizi

Vikundi hewa 851 vyalamba bilioni 2.6 mikopo ya halmashauri

Spread the loveVIKUNDI hewa vya wajasirimali wadogo 851 kutoka katika halmashauri 19...

Habari za SiasaTangulizi

Mashirika matano yapata hasara mabilioni ya fedha

Spread the loveMASHIRIKA matano ya Serikali yanayojiendesha kibiashara, yamepata hasara ya mabilioni...

error: Content is protected !!