Monday , 5 June 2023
Home Gazeti Habari za Siasa CCM yakaa mguu sawa uchaguzi mkuu 
Habari za Siasa

CCM yakaa mguu sawa uchaguzi mkuu 

Spread the love

CHAMA Cha Mapinduzi (CCM) nchini Tanzania, kimeanza rasmi kujipanga kwa ajili ya kushiriki uchaguzi mkuu wa Oktoba 2020. Anaripoti Mwandishi Wetu, Dodoma … (endelea).

Leo Jumatano tarehe 10 Juni 2020, Kamati Kuu ya chama hicho imekutana Ikulu ya Chamwino jijini Dodoma chini ya Mwenyekiti wake, Rais wa Tanzania, John Magufuli.

Taarifa iliyotolewa na Humphrey Polepole, Katibu wa Itikadi na Uenezi wa CCM imesema, kikao hicho pamoja na mambo mengine, kimepokea taarifa ambazo ni; Mpango wa Maandalizi ya Uchaguzi Mkuu wa Mwaka 2020. 

“Kamati Kuu kwa kauli moja imeridhishwa na kiwango cha maandalizi ya kuelekeza Uchaguzi Mkuu na kuelekeza kutolewa maramoja kwa ratiba ya mchakato wa ndani wa uteuzi wa wana CCM wanaoomba kupewa dhamana ya uongozi katika vyombo vya Dola,” amesema Polepole.

Pia, kikao hicho, kimepokea Maandalizi ya Mwelekeo wa Sera za CCM kwa Mwaka 2020 – 2030 na Ilani ya CCM katika Uchaguzi Mkuu wa Mwaka 2020.

“Kamati Kuu imepokea taarifa ya Maendeleo ya Uandishi wa Mwelekeo wa Sera za CCM kwa Mwaka 2020 – 2030 na kujiridhisha kuwa kazi nzuri imefanyika mpaka ngazi ya Rasimu ya Pili.”

“Kamati Kuu pia imepitia kwa mara ya pili Taarifa ya Uandishi wa Ilani ya CCM katika Uchaguzi Mkuu wa Mwaka 2020 na imepongeza Sekretarieti ya Halmashauri Kuu ya Taifa kwa kujumuisha maoni ya wadau mbalimbali na kuelekeza maandalizi ya mwisho ili Ilani hiyo iwasilishwe katika Kikao cha Halmashauri Kuu ya Taifa kwa uamuzi wa mwisho,” amesema

Polepole amesema, kikao kimepokea taarifa ya Serikali juu ya Mapambano ya kuudhibiti ugonjwa wa Corona na hatua ambazo zimechukuliwa kuukabili ugonjwa huo kwa mafanikio makubwa.

“Kikao cha Kamati Kuu (KK) ya Halmashauri Kuu ya Taifa baada ya Tafakuri ya kina juu ya taarifa ya Serikali, kwa kauli moja kimempongeza John Pombe Joseph Magufuli, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa uongozi imara, msimamo thabiti na usioyumba katika kipindi chote cha mapambano dhidi ya ugonjwa huo,” amesema

“Kamati Kuu na kwa niaba ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) inaendelea kutoa rai kwa umma wa Watanzania kuendelea kuzingatia ushauri na maelekezo ya Serikali na wataalam wa Afya, kumtanguliza Mungu kwa maombi na shukrani na kuendelea kuchapa kazi kwa bidii,” amesema

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

Lusinde: CCM hatuliachii ng’o jimbo la Moshi Mjini

Spread the loveMJUMBE wa Halmashauri Kuu ya Chama cha Mapinduzi (NEC), Livingston...

Habari za SiasaTangulizi

Serikali ya Mapinduzi Zanzibar: Bakharesa hajavamia shamba letu

Spread the love  IKULU Visiwani Zanzibar, imeeleza kuwa eneo la kiwanda cha...

Habari za SiasaTangulizi

Zanzibar watangaza rasmi kuwa shamba la Razaba ni mali yao

Spread the love  SERIKALI ya Mapinduzi Zanzibar (SMZ), imetangaza rasmi kwamba shamba...

Habari za SiasaTangulizi

Rais Mwinyi azindua Kamati ya Maridhiano Visiwani

Spread the love  RAIS wa Serikali ya Mapinduzi Zanzibar (SMZ), Dk. Hussein...

error: Content is protected !!