Tuesday , 3 October 2023
Home Gazeti Habari za Siasa CCM yaanza safari kulisaka jimbo la Konde
Habari za Siasa

CCM yaanza safari kulisaka jimbo la Konde

Katibu wa Itikadi na uenezi CCM, Shaka Hamidu Shaka
Spread the love

 

CHAMA Cha Mapinduzi (CCM), kimemteua Sheha Mpemba Faki, kuwa mgombea wake katika uchaguzi mdogo wa Konde, visiwani Zanzibar, unaotarajiwa kufanyika tarehe 18 Julai 2021. Anaripoti Danson Kaijage, Dodoma…(endelea).

Akizungumza na wanahabari leo tarehe 22 Juni 2021, jijini Dodoma, Katibu wa Itikadi na Uenezi CCM, Shaka Hamdu Shaka, amesema Faki ameteuliwa kugombea nafasi hiyo na Kamati Kuu ya Halmashauri Kuu ya Taifa ya chama hicho (NEC).

“Kama mnavyofahamu kuna uchaguzi mdogo katika Jimbo la Konde, mkoani Kaskazini Pemba, tunategemea utafanyika Julai. Upande wa Kamati Kuu imefanya uteuzi wa Faki, atakayesimama katika nafasi ya ubunge wa jimbo hilo,” amesema Shaka.

Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC), iliitisha uchaguzi huo mdogo kufuatia kifo cha aliyekuwa Mbunge wa Konde (ACT-Wazalendo), Khatib Said Haji, kilichotokea tarehe 20 Mei 2021, katika Hospitali ya Taifa Muhimbili, alikokuwa anapatiwa matibabu.

Mwili wa Khatib ulizikwa nyumbani kwao Pemba visiwani Zanzibar, siku hiyo hiyo aliyofariki dunia.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

Bilioni 6.1 kumaliza tatizo la maji Katoro-Buseresere – Geita

Spread the loveMakamu mwenyekiti wa Umoja wa wanawake CCM, (UWT), Zainab Shomari...

Habari za SiasaTangulizi

Serikali kupokea ndege ya 14 ya ATCL, safari kuongezeka

Spread the love  SERIKALI ya Tanzania, kesho tarehe 3 Oktoba 2023, inatarajia...

Habari za Siasa

Serikali yawaangukia viongozi wa dini

Spread the loveSERIKALI imewaomba viongozi wa dini, waendelee kuelimisha wananchi kudumisha amani...

Habari za Siasa

Azzim Dewji aitaka Serikali iwanyooshe mafisadi

Spread the loveMFANYABIASHARA maarufu nchini, Azzim Dewji, ameitaka Serikali iwachukulie hatua wezi...

error: Content is protected !!