WABUNGE watatu wa chama tawala nchini Tanzania- Chama Cha Mapinduzi (CCM), watawekwa ‘kitimoto’ na Kamati ya Maadili ya chama hicho, juu ya tumuma mbalimbali zinazowakabili. Anaripoti Mwandishi Wetu, Dodoma … (endelea).
Wabunge hao ni Askofu Josephat Gwajima (Kawe), Jerry Silaa (Ukonga) na Humphrey Polepole (Kuteuliwa) ambao watafika mbele ya kamati hiyo leo Ijumaa, tarehe 3 Septemba 2021, Makao Makuu ya chama hicho, jijini Dodoma.
Askofu Gwajima wa Kanisa la Ufufuo na Uzima na Silaa, watafika mbele ya kamati wakiwa wanaendelea kutumikia adhabu ya kutohudhuria mikutano miwili ya Bunge, huu unaoendelea na Novemba 2021 na watarejea tena bungeni Januari 2022.
Ni baada ya kukutwa na hatia na Kamati ya Haki, Maadili na Madaraka ya Bunge iliyowahoji Askofu Gwajima na Silaa iliyowahoji kuhusu tuhuma mbalimbali ikiwemo za kusema uongo.
Baada ya kupewa adhabu hiyo, kamati ilishauri mamlaka zingine ikiwemo chama chao- Chama Cha Mapinduzi (CCM) kuwachukulia hatua.
Katibu wa Wabunge wa CCM ambaye pia ni Mbunge wa Mlalo Mkoa wa Pwani, Rashid Shangazi amesema, “tumewaita ili na sisi tuweze kuwahoji na kuwasikiliza katika kikao cha maadili ya chama.”
“Lakini pamoja na waheshimiwa hao Askofu Gwajima na Silaa, tumemwita Polepole naye atakuwa sehemu ya kamati hiyo ya maadili kwa ajili ya mahojiano mbalimbali,” amesema.
Asante kwa kutuhabarisha.
Rafiki yako,
Aliko Musa.
Mbobezi Kwenye Majengo
WATIMUENI HAO KENGE WALIOJIINGIZA KATIKA MAKUNDI YA MAMBA.WASIZIDI KUTUHARIBIA SHUNGULI YA CHAMA NA UONGOZI WA RAIS WETU CHAGUO LA ALLAH MAMA SAMIA SULUH HASSAN. CHAMA KINA KATIBA NA TARATIBU NA MUONGOZO WAKE SIO KILA MTU AWE NA NDEVU KAMA KAMBARE WA MTO KILOMBERO TIMUWENI KABLA HAWAJAAMBUKIZA UGOJWA WA(APEDOMIA) WENGINE.