Friday , 29 March 2024
Home Gazeti Habari za Siasa CCM kuwahoji Askofu Gwajima, Polepole na Silaa
Habari za SiasaTangulizi

CCM kuwahoji Askofu Gwajima, Polepole na Silaa

Askofu Josephat Gwajima
Spread the love

 

WABUNGE watatu wa chama tawala nchini Tanzania- Chama Cha Mapinduzi (CCM), watawekwa ‘kitimoto’ na Kamati ya Maadili ya chama hicho, juu ya tumuma mbalimbali zinazowakabili. Anaripoti Mwandishi Wetu, Dodoma … (endelea).

Wabunge hao ni Askofu Josephat Gwajima (Kawe), Jerry Silaa (Ukonga) na Humphrey Polepole (Kuteuliwa) ambao watafika mbele ya kamati hiyo leo Ijumaa, tarehe 3 Septemba 2021, Makao Makuu ya chama hicho, jijini Dodoma.

Askofu Gwajima wa Kanisa la Ufufuo na Uzima na Silaa, watafika mbele ya kamati wakiwa wanaendelea kutumikia adhabu ya kutohudhuria mikutano miwili ya Bunge, huu unaoendelea na Novemba 2021 na watarejea tena bungeni Januari 2022.

Humphrey Polepole

Ni baada ya kukutwa na hatia na Kamati ya Haki, Maadili na Madaraka ya Bunge iliyowahoji Askofu Gwajima na Silaa iliyowahoji kuhusu tuhuma mbalimbali ikiwemo za kusema uongo.
Baada ya kupewa adhabu hiyo, kamati ilishauri mamlaka zingine ikiwemo chama chao- Chama Cha Mapinduzi (CCM) kuwachukulia hatua.

Katibu wa Wabunge wa CCM ambaye pia ni Mbunge wa Mlalo Mkoa wa Pwani, Rashid Shangazi amesema, “tumewaita ili na sisi tuweze kuwahoji na kuwasikiliza katika kikao cha maadili ya chama.”

“Lakini pamoja na waheshimiwa hao Askofu Gwajima na Silaa, tumemwita Polepole naye atakuwa sehemu ya kamati hiyo ya maadili kwa ajili ya mahojiano mbalimbali,” amesema.

2 Comments

  • WATIMUENI HAO KENGE WALIOJIINGIZA KATIKA MAKUNDI YA MAMBA.WASIZIDI KUTUHARIBIA SHUNGULI YA CHAMA NA UONGOZI WA RAIS WETU CHAGUO LA ALLAH MAMA SAMIA SULUH HASSAN. CHAMA KINA KATIBA NA TARATIBU NA MUONGOZO WAKE SIO KILA MTU AWE NA NDEVU KAMA KAMBARE WA MTO KILOMBERO TIMUWENI KABLA HAWAJAAMBUKIZA UGOJWA WA(APEDOMIA) WENGINE.

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaMakala & Uchambuzi

Nani anasema kuna hasara ATCL?

Spread the loveRIPOTI za makusanyo na matumizi ya fedha katika Kampuni ya...

Habari za SiasaTangulizi

CAG: Wastaafu, wenza wao chanzo NHIF kufilisika

Spread the loveRIPOTI ya ukaguzi ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu...

Habari za SiasaTangulizi

Vikundi hewa 851 vyalamba bilioni 2.6 mikopo ya halmashauri

Spread the loveVIKUNDI hewa vya wajasirimali wadogo 851 kutoka katika halmashauri 19...

Habari za SiasaTangulizi

Mashirika matano yapata hasara mabilioni ya fedha

Spread the loveMASHIRIKA matano ya Serikali yanayojiendesha kibiashara, yamepata hasara ya mabilioni...

error: Content is protected !!