Saturday , 20 April 2024
Home Kitengo Maisha Afya CCBRT wajitosa vita ya corona
Afya

CCBRT wajitosa vita ya corona

Spread the love

MKURUGENZI Mtendaji Mkuu wa hospitali ya CCBRT, Brenda Msangi amekabidhi vifaa maalumu vya kujikinga na virusi vya Corona usoni (Face Shields) vipatavyo 150 kwa hospitali na vituo vya afya 22 katika Manispaa za mkoa wa Dar es Salaam. Anaripoti Hamis Mguta, Dar es Salaam … (endelea).

Akikabidhi visa hivyo leo tare he 27 Mei, 2020, kwa wawakilishi wa hospitali hizo kutoka Manispaa tano za mkoa wa Dar es Salaam, Brenda amesema lengo ni kuunga mkono juhudi za Serikali na wadau wengine hapa nchini katika kuwakinga wahudumu wa afya na janga la Corona. 

“Tumekusudia vifaa hivi vitumike katika vitengo vya afya ya uzazi katika hospitali hizo ili kuwakinga wahudumu wa afya ambao kila siku wamekuwa mstari wa mbele kuokoa maisha ya mama na mtoto,” amesema.

Amesema kuwa vifaa hivyo vitasaidia kuwaweka salama watoa huduma salama wakati wakiwahudumia wagonjwa.

Kwa takribani kipindi cha miaka 10, CCBRT kwa kushirikiana na Timu ya Afya ya Mkoa wa Dar es Salaam (RHMT) na Timu za Afya za Manispaa (CHMTs), wamekuwa wakiendesha mradi wa kujenga uwezo wa watumishi wa afya eneo la afya ya uzazi katika hospitali, vituo vya afya na zahanati 22 katika Manispaa zote tano za Mkoa wa Dar es Salaam.

wa sasa mradi huu pia unafanya kazi na Hospitali ya Taifa ya Muhimbili na Mloganzila hasa kwenye upande wa rufaa za wagonjwa.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

AfyaHabari za Siasa

Serikali yasaka watumishi afya ngazi ya jamii 8,900

Spread the loveSERIKALI imeanza utekelezaji wa mpango jumuishi wa wahudumu wa afya...

AfyaHabari za SiasaTangulizi

Bima ya afya kwa wote kuanza Aprili, wajane kicheko

Spread the loveSHERIA ya Bima ya Afya kwa Wote, inatarajiwa kuanza kutumika...

AfyaHabari Mchanganyiko

Marekani kuipa Tanzania bilioni 980 kudhibiti VVU, UKIMWI

Spread the loveSERIKALI ya Tanzania inatarajiwa kupewa msaada wa fedha kiasi cha...

AfyaHabari Mchanganyiko

Wanavijiji wajenga zahanati kukwepa umbali mrefu kupata huduma

Spread the loveWANAVIJIJI wa Kata ya  Musanja Jimbo la Musoma Vijijini, mkoani...

error: Content is protected !!