Sunday , 10 December 2023
Home Kitengo Maisha Afya CCBRT wajitosa vita ya corona
Afya

CCBRT wajitosa vita ya corona

Spread the love

MKURUGENZI Mtendaji Mkuu wa hospitali ya CCBRT, Brenda Msangi amekabidhi vifaa maalumu vya kujikinga na virusi vya Corona usoni (Face Shields) vipatavyo 150 kwa hospitali na vituo vya afya 22 katika Manispaa za mkoa wa Dar es Salaam. Anaripoti Hamis Mguta, Dar es Salaam … (endelea).

Akikabidhi visa hivyo leo tare he 27 Mei, 2020, kwa wawakilishi wa hospitali hizo kutoka Manispaa tano za mkoa wa Dar es Salaam, Brenda amesema lengo ni kuunga mkono juhudi za Serikali na wadau wengine hapa nchini katika kuwakinga wahudumu wa afya na janga la Corona. 

“Tumekusudia vifaa hivi vitumike katika vitengo vya afya ya uzazi katika hospitali hizo ili kuwakinga wahudumu wa afya ambao kila siku wamekuwa mstari wa mbele kuokoa maisha ya mama na mtoto,” amesema.

Amesema kuwa vifaa hivyo vitasaidia kuwaweka salama watoa huduma salama wakati wakiwahudumia wagonjwa.

Kwa takribani kipindi cha miaka 10, CCBRT kwa kushirikiana na Timu ya Afya ya Mkoa wa Dar es Salaam (RHMT) na Timu za Afya za Manispaa (CHMTs), wamekuwa wakiendesha mradi wa kujenga uwezo wa watumishi wa afya eneo la afya ya uzazi katika hospitali, vituo vya afya na zahanati 22 katika Manispaa zote tano za Mkoa wa Dar es Salaam.

wa sasa mradi huu pia unafanya kazi na Hospitali ya Taifa ya Muhimbili na Mloganzila hasa kwenye upande wa rufaa za wagonjwa.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

AfyaHabari Mchanganyiko

NBC, Taasisi ya Benjamini Mkapa wazindua ufadhili mafunzo ya ukunga kwa wauguzi 50

Spread the loveBenki ya NBC kwa kushirikiana na taasisi ya Benjamin Mkapa...

AfyaHabari za Siasa

RAS Songwe: Tumepigwa… mkurugenzi nakupa siku 21

Spread the loveKATIBU tawala mkoani Songwe, Happines Seneda ametoa siku 21 kwa...

AfyaHabari Mchanganyiko

Majaliwa aipongeza GGML mapambano dhidi ya Ukimwi

Spread the loveWaziri Mkuu Kassim Majaliwa ameipongeza Kampuni ya Geita Gold Mining...

AfyaHabari Mchanganyiko

GGML waungana na Biteko kuanika mbinu za mapambano dhidi ya Ukimwi

Spread the loveNaibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Dk. Doto Biteko...

error: Content is protected !!