Friday , 29 March 2024
Home Kitengo Maisha Elimu CBE yazindua klabu ya ujasiriamali sekondari ya Temeke Wailes
ElimuHabari

CBE yazindua klabu ya ujasiriamali sekondari ya Temeke Wailes

Spread the love
CHUO cha Elimu ya Biashara (CBE), kimezindua klabu ya ujasiriamali kwa shule ya sekondari Temeke Wailes iliyoko Wilaya ya Temeke jijini Dar es Salaam. Anaripoti Mwandishi Wetu…(endelea)

Uzinduzi wa klabu hiyo ulifanyika jana Ijumaa kwenye shule hiyo

Chuo hicho kimesema vilabu hivyo vinalenga kuwawezesha wanafunzi kukua wakifahamu masuala mbalimbali ya biashara tangu utotoni ili waweze kuwa wajasiriamali siku za mbele.

Akizungumza wakati wa uzinduzi wa klabu hiyo Mkurugenzi wa Shahada za Juu, Tafiti na Ushauri wa chuo hicho, Dk. Tumaini Ubadius, alisema wanalenga kuzifikia shule zote za Dar es Salaam.

Dk. Tumaini alisema chuo hicho kimeona ni muhimu wanafunzi wakaanza kufundishwa kuhusu ujasiriamali wakiwa wadogo ili wanapohitimu elimu ya juu wawe na uelewa mpana kuhusu masuala ya biashara.

Wanafunzi wa shule ya Sekondari Wailes iliyoko Temeke jijini Dar es Salam wakionyesha utaalamu waoa wa kutengeneza sabuni shuleni hapo mbele ya viongozi kutoka Chuo cha Elimu ya Biashara (CBE), walipoenda shuleni hapo kufungua klabau ya ujasiriamali.

Alisema kupitia mpango huo, chuo kitakuwa kikipeleka walimu wake kila siku ya Alhamisi kwaajili ya kufundisha wanafunzi wanaosomea mchepuo wa biashara masuala ya ujasiriamali.

“Tunataka kupunguza tatizo la watu kutafuta ajira ili wanapomaliza masomo yao waweze kujiajiri na tunachofanya ni kukuza vipaji na ubunifu walionao tangu wakiwa wadogo,” alisema

“Tumeona tuanze kuwajengea uelewa kuanzia huku chini ili kijana anapokuwa aweze kuwa na ufahamu mazingira yanayomzunguka na changamoto zinazomzunguka kuwa fursa kwake kwa kusaidia jamii na kujiingizia kipato,” alisema

Alisema wamepanga kutembelea shule zote za Dar es Salaam na kuanzisha klabu kama hizo lakini wataenda kwenye mikoa ambayo CBE ina kampasi zake kama Mbeya, Mwanza, Dodoma na Zanzibar.

Mkuu wa shule hiyo, Catherine Mdachi aliushukuru uongozi wa CBE kwa kuichagua shule hiyo kuwa miongoni mwa shule za mwanzo kuwa na klabu hiyo.

“Kuna mkuu wa shule moja alinipigia simu kuniambia hivi kwanini hao CBE wameamua kuja huko na kuja huko kwenu nikawaambia ni habati yetu,” alisema

“Tunamshukuru Rais Samia Suluhu Hassan kwa kuendelea kutujengea madarasa ili watoto wetu wapate sehemu ya kusoma, Huku Temeke hatujui nyota ya kijani tuna watoto wengi lakini tunamshukuru mama ametujengea madarasa mengi,”

Alisema uamuzi huo wa CBE umekuja wakati muafaka kwasababu kuna tatizo kubwa la ajira kwa hiyo kuwafundisha wanafunzi ujasiriamali kutawasaidia kujiajiri kwa kuanzisha biashara zao.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

BiasharaElimu

NMB yatoa vifaa vya ujenzi kwa shule sita Nyasa  

Spread the loveBENKI ya NMB imetoa msaada wa vifaa mbalimbali vya ujenzi...

ElimuHabari Mchanganyiko

GGML yawapa mbinu wanafunzi Geita Boys kufikia malengo ya kitaaluma

Spread the loveKampuni ya Geita Gold Mining Limited (GGML) imetoa mafunzo maalumu...

ElimuHabari Mchanganyiko

Wanawake GGML wawanoa wanafunzi Kalangalala Sec. kujitambua

Spread the loveKATIKA kuadhimisha Siku ya Kimataifa ya Wanawake Duniani, Umoja wa...

ElimuHabari Mchanganyiko

RC Songwe ang’aka kesi 2 kati ya 60 za mafataki kuamuliwa

Spread the loveMkuu wa mkoa wa Songwe Dk. Fransis Michael ameshangazwa na...

error: Content is protected !!