Friday , 19 April 2024
Home Kitengo Michezo Carlinho hati hati mchezo wa Simba na Yanga, Kisinda arejea
Michezo

Carlinho hati hati mchezo wa Simba na Yanga, Kisinda arejea

Spread the love

KIUNGO mshambuliaji wa Yanga C,arlos Carlinho yupo hatihati kuukosa mchezo dhidi ya Simba, kutokana na kuumia kwenye mchezo uliopita wa Kombe la Shirikisho dhidi ya Tanzania Prisons, katika mchezo uliopigwa kwenye Uwanja wa Nelson Mandela, Sumbawanga. Anaripoti Kelvin Mwaipungu, Dar es Salaan … (endelea) 

Mchezo huo utachezwa siku ya Jumamosi tarehe 8 Mei, 2021 kwenye Uwanja wa Benjamin Mkapa jijini Dar es Salaam.

Akitoa taarifa za majeruhi wa timu hiyo kuelekea mchezo wa Jumamos Afisa Habari na mhamasishaji wa klabu ya Yanga, Antonio Nugaz amesema kuwa Carlinho anaendelea na matibabu baada ya kuumia kwenye mchezo dhidi ya Prisons na winga wao Tuisila Kisinda amerejea mara baada ya kukosekana kwenye mchezo uliopita.

Kama Carlinho atakosekana kwenye mchezo huo itakuwa ni mara yake ya tatu kuwa katika majeruhi pale unapokalibia mtanange wa watani wa jadi.

Carlinho alikosa mechi ya mzunguko wa kwanza iliyopigwa kwenye Uwanja wa Benjamin Mkapa ambayo ilimalizika kwa sare ya bao 1-1, na mchezo wa pili ulikuwa ulikuwa visiwani Zanzibar kwenye Fainali ya Kombe la Mapinduzi ambao Yanga waliibuka na ushindi wa penalti 6-5 mara ya kutoka bila kufungana ndani ya dakiak 90.

Kurejea kwa Kisinda aliyeumia bega kwenye mchezo wa Ligi Kuu dhidi ya Biashara ambao Yanga waliibuka na ushindi wa mabao 3-1, imerejesha matumaini kwa mashabiki wa klabu hiyo mara baada ya kufanya vizuri kwenye mchezo uliopita dhidi ya Simba.

Mchezaji huyo anarejea mara baada ya kukosekana kwenye michezo miwili mmoja ukiwa wa Ligi Kuu dhidi ya Azam FC, ambao Yanga walipoteza kwa bao 1-0, na mchezo dhidi ya Prisons.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Michezo

Piga pesa na mechi za EUROPA leo hii

Spread the love Hatimaye Alhamisi ya EUROPA imefika ambapo leo hii mechi...

Michezo

Leo ni leo nani kutinga nusu fainali UEFA?

Spread the love HATIMAYE Jumanne ya UEFA imefika ambapo leo hii michezo...

Michezo

Anza Jumatatu yako na Meridianbet

Spread the love  IKIWA ni siku nyingine mpya kabisa ya Jumatatu baadhi...

Habari MchanganyikoMichezo

NBC, Yanga wazindua kadi  za kimataifa za uanachama

Spread the loveBenki ya Taifa ya Biashara (NBC) kwa kushirikiana na Klabu...

error: Content is protected !!