Friday , 29 March 2024
Home Gazeti Habari CAG: Nyaraka za kughushi zilitumika Jeshi la Zimamoto
Habari

CAG: Nyaraka za kughushi zilitumika Jeshi la Zimamoto

Thobias Andengenye, Mkuu wa jeshi la zimamoto
Spread the love

MDHIBITI na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG), Charles Kichere amesema, nyaraka za fedha za kughushi zimetumika katika Jeshi la Zimamoto na Uokoaji na kuisababisha hasara serikali. Anaripoti Mwandishi Wetu, Dodoma…(endelea).

Amesema, ukaguzi wake kwa mwaka 2019/2020, umebaini akaunti ya masurufu ya jeshi hilo, ilitumika kupitisha malipo batili ya Sh. 261.35 milioni.

Mdhidbiti huyo ametoa taarifa hiyo leo Alhamisi tarehe 8 Aprili 2021, wakati akitoa muhtasari wa ripoti ya ukaguzi kwa mwaka wa fedha wa 2019/2020, jijini Dodoma.

“Nilibaini Sh. 261.35 milioni ziliwekwa kwenye akaunti ya masurufu ya Jeshi la Zimamoto na Uokoaji, katika mojawapo ya benki za biashara kwa vipindi tofauti.”

Charles Kichere, Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG)

“Hata hivyo, Menejimenti ya Jeshi la Zimamoto na Uokoaji haikutambua vyanzo vya fedha hizo na hakukuwa na mawasiliano yoyote yaliyofanywa na benki kuhusuiana na mapokezi ya fedha hizo,” amesema CAG Kichere.

Sambamba na hilo, CAG Kichere amesema, katika ukaguzi wake, alibaini kwamba, kiasi cha fedha hizo zilitolewa na mtunza fedha wa jeshi hilo, kwa kutumia nyaraka za fedha za kughushi.

“Pia, nilibaini kuwa, Kiasi hicho cha fedha kilichukuliwa na mtunza fedha wa Jeshi kutoka katika akaunti hiyo kwa vipindi tofauti, kwa kutumia nyaraka za fedha za kughushi,” amesema CAG Kichere.

Aidha, CAG Kichere amesema alibaini kuwa, usuluhishi wa taarifa za benki kwenye akaunti ya masurufu ya jeshi hilo, haukufanywa kuanzia tarehe 1 Julai 2019 hadi tarehe ya kukamilishwa kwa ukaguzi huo.

“Hii ni kinyume na Kanuni Na. 162 (1) ya Kanuni ya Fedha za Umma ya mwaka 2001 ambayo inahitaji taarifa za fedha za benki, zifanyiwe usuluhisho angalau kila mwezi.

“Hali hii inaashiria udhibiti dhaifu wa mifumo ya ndani kwenye usimamizi wa fedha katika akaunti za benki za Jeshi la Zimamoto na Uokoaji,” amesema CAG Kichere.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

HabariSiasa

Dk. Rose Rwakatare atoa kadi 500 kila Wilaya Morogoro

Spread the loveMWENYEKITI wa Jumuiya ya Wazazi CCM Mkoa wa Morogoro, Dk...

ElimuHabari

CBE, WMA wasaini makubaliano wanafunzi kusoma wakifanyakazi

Spread the loveNAIBU Spika Musa Azzan Zungu amekipongeza Chuo cha Elimu ya...

HabariTangulizi

Dk. Slaa, Mwabukusi kuhojiwa na jeshi la Polisi Mbeya

Spread the loveJESHI la Polisi jijini Mbeya, linawashikilia kwa mahojiano Dk. Wilbroad...

HabariHabari Mchanganyiko

Kairuki Hospital Green IVF  yawanoa madaktari kuhusu upandikizaji mimba

Spread the love KITUO cha Upandikizaji Mimba cha Kairuki Hospital Green IVF...

error: Content is protected !!