PROFESA Mussa Assad, Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG) amewasili bungeni kuitikia wito uliotolewa na Job Ndugai, Spika wa Bunge la Jamhuri wa kukutana na Kamati ya Maadili ya Bunge. Anaripoti Danson Kaijage, Dodoma … (endelea).
Prof. Assad amewasili katika viwanja vya Bunge majira ya saa 4:45 asubuhi ya leo Jumatatu ya tarehe 21 Januari, 2019, tayari kwa mahojiano mbele ya mwenyekiti wa kamati hiyo na kisha kuanza kuhojiwa na wajumbe.
Swali lolote atakaloulizwa kutoka kwa mjumbe yoyote, atatakiwa kulijibu kwa kumuelekea mwenyekiti na sio muuliza swali.
Baada ya mahojiano hayo, Prof. Assad atatakiwa kutoka nje ya ukumbi wa mahojiano ili kutoa nafasi kwa mwenyekiti na wajumbe wa kikao hicho ili kupitia maelezo yake na kama kuna maelezo ya ziata wanayoweza kuyataka kutoka kwake.
Baada ya kikao kupitia nukta kwa nukta na kujiridhisha, Prof. Assad ataitwa tena kwenda kwenye kikao hicho ili kumalizia hatua ya mwisho.
Baada ya kumaliza kikao hicho, itapeleka ripoti yake kwa Spika ikiwa pamoja na mapendekezo yake dhidi ya mtuhumiwa. Spika naye atakuwa na hiyari ya kusoma bungeni uamuzi uliofikiwa ama wabunge kupendekeza adhabu.
Leave a comment