Sunday , 26 March 2023
Home Gazeti Habari Mchanganyiko CAG: ATCL imetengeneza hasara ya bilioni 60
Habari Mchanganyiko

CAG: ATCL imetengeneza hasara ya bilioni 60

Ndege ya Shirika la Ndege Tanzania (ATCL)
Spread the love

 

SHIRIKA la Ndege Tanzania (ATCL), limetengeza hasara katika kipindi cha miaka mitano, ambapo mwaka huu, limetengeza hasara ya Sh. 60 bilioni. Anaripoti Regina Mkonde, Dar es Salaam…(endelea).

Taarifa hiyo imetolewa leo Jumapili tarehe 28 Machi 2021, na Mdhibiti na Mkaguzi wa Hesabu za Serikali (CAG), Charles Kichere, wakati anawasilisha ripoti yake ya ukaguzi wa hesabu za Serikali kwa mwaka wa fedha wa 2019/2020, Ikulu jijini Dodoma.

CAG Kichere amewasilisha ripoti hiyo kwa Rais Samia Suluhu Hassan.

“Shirika letu la ndege nimegundua limetengeza hasara , mwaka huu limetengeza hasara Sh. 60 bilioni, lakini kwa miaka mitano limekuwa likitengeneza hasara pia,” amesema CAG Kichere.

CAGKichere amesema hayo wakati anaeleza muhtasari wa ukaguzi uliofanywa katika mashirika ya umma, ambapo amesema pia, amebaini ubadhirifu katika Mamlaka ya Bandari Tanzania (TPA).

Mdhibiti huyo na mkaguzi wa hesabu za serikali amesema ofisi yake inaendelea kukagua ubadhirifu huo, huku akiiomba Serikali ya Rais Samia kuzifanyia kazi changamoto hizo.

“Ukaguzi tuliofanya katika mashirika mbalimbali ya Serikali, tumegundua changamoto kadhaa ambazo zinahitaji serikali kukagua, ikiwemo matatizo katika Shirika la Bandari, ubadhirifu ambao tunaendelea kufanya ukaguzi katika maeneo hayo,” amesema CAG Kichere

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

Mchina wa SGR aburuzwa kortini kwa kumjeruhi Mtanzania, TRC waja juu

Spread the love  RAIA wa China, Zheng Yuan Feng, amefikishwa mahakamani kwa...

Habari Mchanganyiko

Watendaji Kata, Mitaa watakaoshindwa kusimamia usafi kukiona

Spread the love  WATENDAJI wa kata, mitaa na vitongoji na maofisa afya...

Habari Mchanganyiko

Mtia nia urais TLS kukata rufaa kupinga kuenguliwa

Spread the love  MTIA nia ya kugombea Urais wa Chama cha Mawakili...

Habari Mchanganyiko

NBC yazindua kampeni ya mkeka wa ushindi na ATM zake

Spread the loveBENKI ya Taifa ya Biashara (NBC) imetangaza uzinduzi wa kampeni...

error: Content is protected !!