Thursday , 25 April 2024
Home Habari Mchanganyiko CAG: ATCL imetengeneza hasara ya bilioni 60
Habari Mchanganyiko

CAG: ATCL imetengeneza hasara ya bilioni 60

Ndege ya Shirika la Ndege Tanzania (ATCL)
Spread the love

 

SHIRIKA la Ndege Tanzania (ATCL), limetengeza hasara katika kipindi cha miaka mitano, ambapo mwaka huu, limetengeza hasara ya Sh. 60 bilioni. Anaripoti Regina Mkonde, Dar es Salaam…(endelea).

Taarifa hiyo imetolewa leo Jumapili tarehe 28 Machi 2021, na Mdhibiti na Mkaguzi wa Hesabu za Serikali (CAG), Charles Kichere, wakati anawasilisha ripoti yake ya ukaguzi wa hesabu za Serikali kwa mwaka wa fedha wa 2019/2020, Ikulu jijini Dodoma.

CAG Kichere amewasilisha ripoti hiyo kwa Rais Samia Suluhu Hassan.

“Shirika letu la ndege nimegundua limetengeza hasara , mwaka huu limetengeza hasara Sh. 60 bilioni, lakini kwa miaka mitano limekuwa likitengeneza hasara pia,” amesema CAG Kichere.

CAGKichere amesema hayo wakati anaeleza muhtasari wa ukaguzi uliofanywa katika mashirika ya umma, ambapo amesema pia, amebaini ubadhirifu katika Mamlaka ya Bandari Tanzania (TPA).

Mdhibiti huyo na mkaguzi wa hesabu za serikali amesema ofisi yake inaendelea kukagua ubadhirifu huo, huku akiiomba Serikali ya Rais Samia kuzifanyia kazi changamoto hizo.

“Ukaguzi tuliofanya katika mashirika mbalimbali ya Serikali, tumegundua changamoto kadhaa ambazo zinahitaji serikali kukagua, ikiwemo matatizo katika Shirika la Bandari, ubadhirifu ambao tunaendelea kufanya ukaguzi katika maeneo hayo,” amesema CAG Kichere

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

Exim Bank yatoa  vitanda kwa shule ya Jeshi la Polisi Moshi

Spread the love  BENKI ya Exim imekabidhii  seti ya vitanda kwa Shule...

Habari Mchanganyiko

NBC yakabidhi vitanda Shule ya Polisi Moshi

Spread the loveBenki ya NBC imekabidhi msaada wa vitanda 28 kwa Shule...

Habari Mchanganyiko

THRDC yaongeza mkataba wa ushirikiano na ABA

Spread the love  MTANDAO wa Watetezi wa Haki za Binadamu Tanzania (THRDC),...

Habari Mchanganyiko

Rufaa ya Equity Benki, State Oil yakwama

Spread the loveMAHAKAMA ya Rufani, jijini Dar es Salaam, imeshindwa kuendelea na...

error: Content is protected !!