Thursday , 30 March 2023
Habari za Siasa

CAG apekua BoT

Benki Kuu ya Tanzania (BoT)
Spread the love

 

FEDHA zilizotolewa Benki Kuu ya Tanzania (BoT) na kutumika kati ya Januari na Machi mwaka huu, zimeanza kuchunguzwa. Anaripoi Mwandishi Wetu, Dar es Salaam … (endelea).

Hatua hiyo inatokana na agizo la Rais Samia Suluhu Hassan, kuagiza Ofisi ya Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (Takururu) pia Ofisi ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG), kupitia mafaili ya matumizi ya fedha hizo.

Rais Samia alitoa maagizo hayo tarehe 28 Machi 2021, wakati akipokea taarifa ya CAG na ya utendaji wa Takukuru kwa mwaka 2019/2020.

Charles Kichere, Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG)

Akizungumza na gazeti moja la kila siki nchini, CAG Charles Kichere amesema, tayari wameanza uchunguzi BoT ikiwa ni kutekeleza agizo la Rais Samia.

“Tunaendelea na ukaguzi. Siwezi kusema kilichofanyika hadi sasa tupo site (eneo la tukio), tunaendelea na ukaguzi,” CAG Kichere amelieleza gazeti hilo.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

TEMESA iliyokarabati Kivuko kwa Bil 7.5 yapata hati chafu

Spread the love  MDHIBITI na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG),...

Habari za Siasa

ACT-Wazalendo yakusanya Mil 8.5/- kodi ya zuio na kutokomea nazo

Spread the love  MDHIBITI na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG),...

Habari za Siasa

DC Kasilda Mgeni ahamasisha chakula shuleni

Spread the love  MKUU wa Wilaya ya Same, mkoani Kilimanjaro, Kasilda Mgeni...

Habari za Siasa

Bilioni 223.9 zapelekwa Tunduru ndani ya miaka 2 ya SSH

Spread the love  ZAIDI ya Sh. bilioni 223.9 zimepelekwa Wilaya ya Tunduru...

error: Content is protected !!