Thursday , 30 March 2023
Home Kitengo Maisha Elimu Bweni lamuweka matatani Mkuu wa Shule Naliendele
Elimu

Bweni lamuweka matatani Mkuu wa Shule Naliendele

David Silinde, Naibu Waziri wa Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI)
Spread the love

 

HALIDI Mchanga, Mkuu wa Shule ya Sekondari ya Naliendele, amesimamishwa kazi kwa kushindwa kukamilisha mradi wa bweni na bwalo la chakula katika shule hiyo. Anaripoti Mwandishi Wetu, Mtwara … (endelea).

Hatua hiyo imechukuliwa na David Silinde, Naibu Waziri wa Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI), baada ya kutembelea shule hiyo iliyopo katika Halmashauri ya Manispaa ya Mtwara Mikindani, Mtwara.

Silinde amesema, kwenye shule hiyo amekuta matumizi mabaya ya fedha ambazo zilipaswa kuelekezwa kwenye ujenzi huo uwe ambao ulipaswa kukamilika mwishoni mwa mwaka jana 2020.

Waziri huyo amesema, ujenzi huo umesimama licha ya Sh. 180 milioni zilizotolewa na serikali kuelezwa kwamba zimekwisha.

Mchanga amemweleza Silinde kwamba walikutana na changamoto ya upatikanaji wa saruji, mvua kubwa kukwamisha ujenzi.

Na kwamba, walilazimika wasubiri mvua ziishe mwanzoni mwa mwaka huu, pia ameeleza ushiriki hafifu wa wananchi katika kuchangia ujenzi ikiwemo kuchimba msingi, kumechangia.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

ElimuHabari

Serikali yataka vijana  wajiunge na program atamizi ya biashara CBE

Spread the love  SERIKALI imewahamasisha vijana kujiunga na program atamizi inayotolewa na...

Elimu

Mfuko wa Jimbo Musoma Vijijini wamwaga mamilioni ujenzi maabara za sekondari

Spread the love  MFUKO wa Jimbo la Musoma Vijijini, Mkoa wa Mara,...

ElimuHabari

CBE yaanzisha Shahada 10 za Uzamili, CBE yajivunia wahitimu wanaoajirika

Spread the loveCHUO cha Elimu ya Biashara (CBE), kimewataka wenye  kampuni na...

Elimu

Harambee ujenzi sekondari za Musoma Vijijini yashika kasi

Spread the love  HARAMBEE ya ujenzi na ukarabati wa shule za sekondari...

error: Content is protected !!