ALIYEKUWA Mbunge wa Kilwa Kusini kupitia Chama Cha Wananchi (CUF), Selemani Bungara maarufu ‘Bwege’ ametoa msimamo wake wa kisiasa mara baada ya kushindwa ubunge katika uchaguzi uliofanyika tarehe 28 Oktoba 2020. Anaripoti Hamis Mguta, Kilwa … (endelea).
Bwege ameongoza Jimbo hilo kwa miaka kumi mfululizo akiwa CUF, lakini katika uchaguzi mkuu uliopita, alikuwa akitetea nafasi hiyo kupitia ACT-Wazalendo.
MwanaHALISI Online, limemtembelea Bwege, nyumbani kwake Kilwa Kivinje Mkoa wa Lindi na kuzungumza naye masuala mbalimbali.
Bwege ambaye anakumbukwa akiwa bungeni kuibua misemo mbalimbali ukiwemo ‘We ulisikia wapi?” au “Tunaanza upya” amegusua hatima yake ya kisiasa.
Haya na mengine mengi endelea kutazama mahojiano hayo hapo chini.
Grazie time is over