Friday , 29 March 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Butiku ataka nguvu ielekezwe kwenye maendeleo ya wananchi kuliko vyama
Habari za Siasa

Butiku ataka nguvu ielekezwe kwenye maendeleo ya wananchi kuliko vyama

Mrugenzi wa Taasisi ya Mwalimu Nyerere, Mzee Joseph Butiku
Spread the love

 

MKURUGENZI wa Taasisi ya Mwalimu Nyerere, Mzee Joseph Butiku, ameishauri Serikali na jamii, kujikita katika mipango ya maendeleo ya wananchi, badala ya kuelekeza nguvu kwenye siasa, ili kudumisha mfumo wa vyama vingi nchini. Anaripoti Mwandishi Wetu, Dar es Salaam … (endelea).

Mzee Butiku ametoa maoni hayo leo Ijumaa, tarehe 1 Julai 2022, akitoa ujumbe wake kuhusu maadhimisho ya miaka 30 ya mfumo wa vyama vingi vya siasa, baada ya kuwasilisha mapendekezo yake juu ya uboreshaji wa demokrasia na mifumo ya sheria, katika Kikosi Kazi cha Rais, jijini Dar es Salaam.

“Tukijielekeza fikra, kauli na mawazo ya mipango yetu katika kuhudumia watu wetu, kuwawezesha waendelee kiuchumi, waelewe vizuri nchi yao kisiasa, watumie maisha na misingi yao kujenga umoja na amani yetu,” amesema Mzee Butiku.

Mzee Butiku amesema “tukienda na mambo ya wananchi tukaelekeza nguvu zetu huko kuliko nguvu kwenye vyama kinadharia, nadhani tutakwenda vizuri.”

Mwanasiasa huyo mkongwe nchini Tanzania, amesema Rais aliyeko madarakani, Samia Suluhu Hassan, anajitahidi katika kutekeleza masuala hayo.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

Chadema yamtaka Rais Samia aunde tume kuchunguza mauaji mgodi wa Barick

Spread the loveRAIS Dk. Samia Suluhu Hassan, ameombwa aunde tume huru kwa...

Habari za SiasaMakala & Uchambuzi

Nani anasema kuna hasara ATCL?

Spread the loveRIPOTI za makusanyo na matumizi ya fedha katika Kampuni ya...

Habari za SiasaTangulizi

CAG: Wastaafu, wenza wao chanzo NHIF kufilisika

Spread the loveRIPOTI ya ukaguzi ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu...

Habari za SiasaTangulizi

Vikundi hewa 851 vyalamba bilioni 2.6 mikopo ya halmashauri

Spread the loveVIKUNDI hewa vya wajasirimali wadogo 851 kutoka katika halmashauri 19...

error: Content is protected !!