SERIKALI imeshauriwa kufanya tathimini ya kina kabla ya kuomba ahirisho la kulipa madeni ya Serikali. Anaripoti Mwandishi Wetu, Dodoma … (endelea).
Serikali ipo kwenye mazungumzo na nchi wanachama wa Paris (Paris Club) na wasio wanachama na zile zilizoikopesha kwa njia ya billateral ili kuangalia namna ya kuahirisha ulipaji wa madeni katika kipindi hiki ambacho hali ya ukuaji wa uchumi umeathiriwa na janga la Uviko-19 na vita vya Urusi na Ukrenia.
Akisoma taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Bajeti, leo Jumanne tarehe 7 Juni, 2022, Makamu Mwenyekiti wa Kamati hiyo, Omary Kigua, amesema jambo hilo lina mitazamo miwili.
Amesema mtazamo wa kwanza ni kuwa hatua hii itatoa ahueni kwenye bajeti na kuiwezesha Serikali kufanya miradi mingine huku upande mwingine ikiwa ni edapo Serikali itakua na mapato ya kutosha kulipa pindi madeni hayo yatakapoiva.
“Muda wa kulipa ukifika lazima mapato yawepo na uwezo wa kubeba madeni yaliyoiva ya wakati huo na yaliyoahirishwa,” amesema na kuongeza;
“Lazima Serikali ifanye tathimini ya kina na kuangalia endapo mapato yataweza kubeba mzigo huo kabla ya kuomba ahirisho.”
Ameongeza pia kuwa Serikali itafute namna itakavyoweza kuongeza mapato ya fedha za kigeni ili deni la Serikali kuendelea kuwa himilivu, “mfano kutumia vyanzo bunifu vya fedha kama infrastructure bond, carbon credit.”
Leave a comment