Thursday , 25 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Bunge lina ugeni mzito – Spika Ndugai
Habari za Siasa

Bunge lina ugeni mzito – Spika Ndugai

Job Ndugai Spika wa Bunge la jamhuri ya muungano wa Tanzania
Spread the love

 

JOB Ndugai, Spika wa Bunge la Jamhuri amewaeleza wabunge wa bunge hilo kwamba, kesho Alhamis tarehe 22 Aprili 2021, kutakuwa na ugeni mzito. Anaripoti Danson Kaijage, Dodoma … (endelea).

Amesema, Rais Samia Suluhu Hassan atahutubia Bunge kama ilivyoelezwa awali na kwamba, si vizuri wabunge wakiwemo mawaziri na manaibu waziri kutokuwepo bungeni.

Akisisitiza uwepo wa wabunge wote, Spika Ndugai ameshauri wabunge wawaangalie wabunge wenzao na kama hawapo, wawapigie simu wasafiri usiku kwenda Dodoma.

“Kesho tutakuwa na ugeni mkubwa sana, Rais wa Awamu ya Sita anakuja kulihutubia Bunge. Huwezi kujua kesho wala kesho kutwa, si vizuri kutokuwepo kwenye Landmark ya mheshimiwa Rais wa awamu wa sita anapokuja kulihutubia Bunge hili,” amesema Spika Ndugai huku akisitiza, haipendezi gallery kujaa halafu ukumbi wa bunge kuwa wazi.

Rais Samia ambaye ni Rais wa Sita wa Tanzania, aliapishwa tarehe 19 Machi 2021 kuwa rais ikiwa ni siku mbili baada ya kutangazwa kifo cha mtangulizi wake, Hayati John Magufuli.

Rais Samia kesho tarehe 22 Aprili 2021, atalihutubia Bunge kwa mara ya kwanza tangu aapishwe kuwa kiongozi mkuu wa nchi.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

Kilosa yawa mfano wa kuigwa miradi ya Mwenge nchini

Spread the love  KIONGOZI wa Mbio za Mwenge Kitaifa Godfrey Mzava amezitaka...

Habari za SiasaTangulizi

Biteko ataja vipaumbele 7 bajeti nishati 2024/25

Spread the love  NAIBU Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Dk. Doto...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Mwekezaji amwaga bil. 39 kujenga viwanda 3 vya uchenjuaji

Spread the loveKampuni ya Mineral Access System Limited (MAST) inayoiwakilishwa kampuni ya...

Habari za SiasaTangulizi

Mpwa wa Magufuli mbaroni kwa kusambaza picha za utupu

Spread the loveJESHI la Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam limewakamata...

error: Content is protected !!