Saturday , 20 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Bunge lawatia kifungoni Askofu Gwajima, Silaa hadi 2022
Habari za SiasaTangulizi

Bunge lawatia kifungoni Askofu Gwajima, Silaa hadi 2022

Spread the love

 

WABUNGE  wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Askofu Josephat Gwajima (Kawe) na Jerry Silaa (Ukonga), wamepewa adhabu ya kutohudhuria mikutano miwili mfululizo  ya Bunge, baada ya kukutwa na hatia katika makosa ya kudharau na kudhalilisha mhimili huo. Anaripoti Regina Mkonde, Dar es Salaam … (endelea).

Adhabu hiyo imetolewa leo Jumanne, tarehe 31 Agosti 2021, bungeni jijini Dodoma,  baada ya wabunge kuunga mkono adhabu zilizopendekezwa na Kamati ya Maadili, Haki na Madaraka ya Bunge, dhidi ya wabunge hao.

Akizungumza baada ya kuwahoji wabunge dhidi ya hoja ya kamati hiyo kuhisi adhabu ilizopendekeza dhidi ya wabunge hao, Spika wa Bunge Job Ndugai, amesema adhabu hizo ni ndogo.

Na kwamba kama wataendelea kufanya vitendo vya utovu wa nidhamu, watachukuliwa hatua zaidi.

“Bunge lote limeafiki kabisa adhabu zile na adhabu hizi zimetolewa kwa kweli ni ndogo sana,  huo ni ukweli kwa makosa waliyotenda sababu ni mikutano miwili na maana yake huu unahesabika kiukweli  wanakosa huo unaokuja. tunasikitika ni ndogo mnajua kanuni zinaruhusu kutoa adhabu nyingine zaidi ya hivyo. Tutakuwa tayari kufanya hivyo wakitulazimisha kufanya hivyo,” amesema Spika Ndugai.

Kwa mujibu wa Spika Ndugai,  adhabu yao itaishia katika mkutano wa tano na wataanza kuhudhuria mkutano wa sita utakaoanza  utakaoanza Januri 2022.

Awali, kamati hiyo ilipendekeza wabunge hao wasimamishwe kuhudhuria mikutano miwili na au mitatu mfululizo, baada ya kuwakuta na hatia walipohojiwa.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

BiasharaHabari za Siasa

Mavunde aagiza Perseus kuharakisha fidia Sengerema

Spread the loveWaziri wa Madini, Anthony Mavunde ameipongeza Kampuni ya Perseus kwa...

Habari za Siasa

Kigogo Chadema awanyooshea vidole vigogo serikalini kuhusu ripoti ya CAG

Spread the love  MWANACHAMA wa Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Boniface Jacob, amedai...

Habari za Siasa

Wabunge waikalia kooni TAKUKURU Bungeni

Spread the love  BAADHI ya wabunge wamelia na changamoto za utendaji wa...

Habari za SiasaTangulizi

Mpina ataka Waziri Majaliwa ajiuzulu, akosoa teuzi za mawaziri

Spread the love  MBUNGE wa Kisesa, Luhaga Mpina, amemtaka Waziri Mkuu, Kassim...

error: Content is protected !!