Thursday , 25 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Bunge lamuweka rehani Waziri Tizeba
Habari za SiasaTangulizi

Bunge lamuweka rehani Waziri Tizeba

Dk. Charles Tizeba, Waziri wa Kilimo
Spread the love

BAJETI ya Wizara ya Kilimo iliyowasilishwa bungeni mjini Dodoma jana Jumanne, ni mzigo kwa wananchi na imelenga kuwanyonya wakulima. Anaripoti Faki Sosi … (endelea).

Akichangia mjadala wa bajeti ya wizara hiyo, mbunge wa Mbozi (Chadema), Pascal Haonga, ametuhumu serikali kunyonya wakulima na kupendelea wafanyabiashara.

“Hii serikali haina dira yeyote kwenye sekta ya kilimo. Haina mkakati wala mipango ya kusaidia wakulima. Kinachoonekana ni kwamba serikali imejipanga kupunja wakulima kupitia vyama vya ushirika,” ameeleza.

Amesema, “kuna watu wamefilisi vyama hivi vya ushirika, lakini hawajachukuliwa hatua. Leo serikali inafufua tena vyama hivi ambavyo vimekuwa mzigo kwa wananchi wetu bila kutuambia waliofilisi ushirika wamefanywa nini.”

Naye Nape Nnauye, mbunge wa Mtama (CCM), amedai kuwa bajeti hiyo haina jipya na hivyo inapaswa kuondolewa bungeni.

Amesema, “serikali isionea aibu kuiondoa bungeni bajeti ya wizara hii ili ikajipange upya. Hii bajeti itaiumiza wananchi wetu na hivyo kuiweka serikali ya chama changu kwenye wakati mgumu wa kujitetea.”

Nape amehoji mahali ambako mabilioni ya shilingi ambayo serikali imekuwa ikijigamba kuwa imekusanya yalikohifadhiwa.

Amesema, “umefika wakati wa kuelezana ukweli kuwa bajeti ya wizara hii ni ngumu na haiendani kabisa la Ilani ya uchaguzi ya CCM, ikipitishwa itakuwa mwiba kwa serikali. Namuonea huruma waziri wa kilimo, Dk. Charles Tizeba kwa kuwa kuna mambo yako nje ya uwezo wake, lakini kila jambo anabebeshwa yeye.”

Amesema, “bajeti inagusa asimilia 80 ya wananchi na inagusa maisha ya watu wetu. Serikali inajali maendeleo ya vitu au watu waliowaweka madarakani jambo ambalo majibu yake yatakuwa na maana tofauti kwa wananchi.”

Amesema serikali haiwajali wakulima kwa maelezo kuwa imekuwa ikipunguza bajeti hiyo kuanzia mwaka 2018/17.

“Wakati fulani tulisema Serikali ikwepe kuwekeza fedha nyingi kwenye miradi mikubwa inayoweza kujiendesha kibiashara, lakini tukashambuliwa kama si wazalendo katika nchi hii, na hili Tizeba tutakubebesha bure lakini si lako,” ameeleza Nape.

Amesema akikubali bajeti hiyo, wananchi wake wa Mtama na wakulima wa korosho, ufuta, pamba na mazao mengine nchini watamshangaa kwa kiasi kikubwa hivyo hakuna shida wala aibu kukaa pamoja na kuifumua kama ilivyowahi kufanyika kwa wizara nyingine.

Akizungumzia Ilani ya uchaguzi ya CCM, Nape ambaye aliwahi kuwa katibu mwenezi wa chama hicho amesema, “ilani ilitamka kuwa Serikali itakayoundwa itakuwa na jukumu la kuwasaidia wakulima kutafuta masoko ya nje lakini kwa sasa imekuwa kinyume kabisa na ilani hiyo, kwamba kukaa mezani ndio suluhu.

“Ukimwambia mtu akale magunia 20 ya mbaazi si unamtukana huyu, hivi tunawaambia nini wakulima katika jambo hili, ni kwa nini tusiwe wepesi wa kukubali ushauri na kuzungumza kwa pamoja. Naomba sana, bajeti hii iondolewe kwa kuwa haikidhi mahitaji ya sasa.”

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

Prof. Muhongo akomalia matumizi nishati jadidifu kuondoa uhaba wa umeme

Spread the love  MBUNGE wa Musoma Vijijini (CCM), Profesa Sospeter Muhongo, ameendelea...

Habari za Siasa

Kilosa yawa mfano wa kuigwa miradi ya Mwenge nchini

Spread the love  KIONGOZI wa Mbio za Mwenge Kitaifa Godfrey Mzava amezitaka...

Habari za SiasaTangulizi

Biteko ataja vipaumbele 7 bajeti nishati 2024/25

Spread the love  NAIBU Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Dk. Doto...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Mwekezaji amwaga bil. 39 kujenga viwanda 3 vya uchenjuaji

Spread the loveKampuni ya Mineral Access System Limited (MAST) inayoiwakilishwa kampuni ya...

error: Content is protected !!