Saturday , 20 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Bunge lamtia hatiani Gwajima
Habari za SiasaTangulizi

Bunge lamtia hatiani Gwajima

Askofu Josephat Gwajima
Spread the love

 

KAMATI ya Haki, Maadili na Madaraka ya Bunge, leo tarehe 31 Agosti, 2021, imemtia hatiani Mbunge wa Kawe, Askofu Josephat Gwajima (CCM) kwa makosa ya kudhalilisha, kuchonganisha Bunge na mihimili mingine, Serikali na wananchi. Anaripoti Mwandishi Wetu, Dodoma … (endelea).

Akiwasilisha taarifa ya kamati hiyo kuhusu uchunguzi wa tuhuma zilizokuwa zinamkabili Gwajima, Mwenyekiti wa kamati hiyo, Emmanuel Mwakasaka amesema kamati imependekeza vyombo vya kisheria vifuatilie mienendo ya Askofu Gwajima.

Alisema kwa kuwa Askofu Gwajima alikiri kauli zote zilizolalamikiwa kuwa ni za kwake, Kamati imependekeza Bunge liazimie kumpa adhabu ya kutohudhuria mikutano miwili ya Bunge.

“Kuna viashiria vya uwepo wa jinai na uvunjifu wa amani. Pia suala hili lishughulikiwe kwa mujibu wa kanuni na maadili ya viongozi wa umma sambamba na chama chake CCM kimchukulie hatua,” alisema Mwakasaka.

Alisema licha ya Gwajima kutakiwa kutoa ushahidi wa tuhuma alizozitoa, hakuwa na vielelezo vyovyote vya kuhusu kauli alizozitoa ikiwamo kutuhumu viongozi wa serikali kupewa hela ili kuruhusu chanjo iletwe nchini.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

Dk. Mwakyembe : Zanzibar waliongoza kutaka Serikali 2 za muungano

Spread the love  MWANASIASA mkongwe nchini, Dk. Harrison Mwakyembe, amesema mjadala wa...

Habari za SiasaTangulizi

Rais Samia ataja mikakati ya kufikia trilioni 2 biashara Uturuki, Tz

Spread the loveWakati Tanzania na Uturuki zikidhamiria kuongeza kiwango cha biashara hadi...

BiasharaHabari za Siasa

Mavunde aagiza Perseus kuharakisha fidia Sengerema

Spread the loveWaziri wa Madini, Anthony Mavunde ameipongeza Kampuni ya Perseus kwa...

Habari za Siasa

Kigogo Chadema awanyooshea vidole vigogo serikalini kuhusu ripoti ya CAG

Spread the love  MWANACHAMA wa Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Boniface Jacob, amedai...

error: Content is protected !!