Thursday , 30 March 2023
Home Gazeti Habari za Siasa Bunge laagiza uchunguzi MOI
Habari za Siasa

Bunge laagiza uchunguzi MOI

Hospitali ya Muhimbili kitengo cha Mifupa (MOI)
Spread the love

 

BUNGE la Tanzania, limeiagiza Serikali, ifanye uchunguzi wa mifumo inayoratibu shughuli za kitabibu na hesabu za Taasisi ya Mifupa ya Muhimbili (MOI). Anaripoti Mwandishi Wetu, Dar es Salaam…(endelea).

Agizo hilo limetolewa leo Alhamisi, tarehe 10 Juni 2021, bungeni jijini Dodoma na Spika wa Bunge, Job Ndugai, akisoma mapendekezo ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Hesabu za Serikali (PAC).

Kuhusu mashirika yaliyoshindwa kuwasilisha kwa Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG), taarifa za hesabu kwa mwaka 2019/2020, kwa ajili ya ukaguzi.

Bunge limeagiza uchunguzi huo, baada ya MOI kushindwa kukamilisha hesabu zake kwa mwaka huo wa fedha, kufuatia taarifa za mifumo hiyo kutolingana.

Job Ndugai, Spika wa Bunge Tanzania

Kufuatia changamoto hiyo, Spika Ndugai amesema, bunge linaishauri Serikali ifanye uchunguzi wa mchakato mzima wa ununuzi na usimikaji wa mfumo wa shughuli za kitabibu, wa taasisi hiyo.

“Kuhusu MOI kutokukamilisha hesabu, kutokana na changamoto ya mfumo wa kitabibu kutowasiliana ipasavyo na mfumo wa hesabu. Tunashauri Serikali ifanye uchunguzi wa mchakato mzima wa ununuzi na usimikaji, mfumo wa shughuli za kitabibu uliopo MOI,” amesema Spika Ndugai.

Kiongozi huyo wa Bunge ameongeza “kubaini iwapo taratibu zilifuatwa na kama mfumo huo una manufaa kwa Taifa.”

Wakati huo huo, Spika Ndugai ameishauri Serikali ipeleke watalaamu wenye sifa katika taasisi hiyo, kwani MOI ina tatizo la ukosefu wa wahasibu wasio na vigezo.

“Aidha, Serikali ipeleke wataalamu wenye sifa MOI kutekeleza shughuli za ukaguzi na uhasibu. Tunapata shida ya wahasibu MOI kutokana na sifa zao, tupate ambao ni more qualify (wanaokidhi vigezo),” amesema Spika Ndugai.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

TEMESA iliyokarabati Kivuko kwa Bil 7.5 yapata hati chafu

Spread the love  MDHIBITI na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG),...

Habari za Siasa

ACT-Wazalendo yakusanya Mil 8.5/- kodi ya zuio na kutokomea nazo

Spread the love  MDHIBITI na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG),...

Habari za Siasa

DC Kasilda Mgeni ahamasisha chakula shuleni

Spread the love  MKUU wa Wilaya ya Same, mkoani Kilimanjaro, Kasilda Mgeni...

Habari za Siasa

Bilioni 223.9 zapelekwa Tunduru ndani ya miaka 2 ya SSH

Spread the love  ZAIDI ya Sh. bilioni 223.9 zimepelekwa Wilaya ya Tunduru...

error: Content is protected !!