Friday , 29 September 2023
Home Kitengo Habari Kimataifa Bunge la Uganda giza kama Tanzania
Kimataifa

Bunge la Uganda giza kama Tanzania

Godfrey Mutabazi, Mkurugenzi wa Tume ya Utangazaji Uganda
Spread the love

VYOMBO vya habari nchini Uganda vimezuiwa kuonesha matangazo ya moja kwa moja (Mubashara) vikao vya Bunge vinavyoendelea nchini Uganda, anaandika Hamis Mguta.

Mkurugenzi wa Tume ya Utangazaji nchini humo, Godfrey Mutabazi amesema redio na televisheni zote haziruhusiwi kurusha matangazo ya Bunge moja kwa moja kuanzia leo Alhamisi.

Amesema Bunge limeamua kutoonyeshwa moja kwa moja kwa matangazo hayo kutokana na sababu za kiusalama.

Mapema leo, wabunge nchini humo wamepigana ndani ya ukumbi wa bunge wakiwa katika siku ya pili ya kikao cha kujadili muswada wa kuondoa ukomo wa miaka ya kugombea nafasi ya urais kwa mujibu wa katiba ya taifa hilo.

Ugomvi huo ulianza pale Spika alipochukua hatua ya kuwafukuza wabunge wapatao 25 wengi wao wakiwa ni wale wa upinzani kwa madai ya utovu wa nidhamu pamoja na Waziri wa serikali aliyeshtakiwa kwa kufyatua risasi bungeni siku ya Jumanne.

Wabunge wa Chama tawala nchini humo wamefanikiwa kuwasilisha ombi la kuandaa mswada wa kubadilisha katiba na kuondoa kifungu kinachozuia mtu kuwania urais akiwa na umri wa zaidi ya miaka 75.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Kimataifa

Mahakama yamkuta na hatia Donald Trump

Spread the love  ALIYEKUWA Rais wa Marekani, Donald Trump, amekutwa na hatia...

Kimataifa

Harusi yageuka msiba 100 wakifariki kwa ajali ya moto

Spread the love  WATU takribani 100, akiwemo bibi na bwana harusi, wamefariki...

Kimataifa

Kampuni ya mali ya China Oceanwide yapata agizo la kufilisiwa huko Bermuda

Spread the love  MAHAKAMA ya Bermuda imetoa amri ya kufilisiwa kwa Kamapuni...

Kimataifa

Uvamizi wa kijeshi Milango ya bahari ya Taiwan G7 yapinga China

Spread the loveMKUTANO wa Mawaziri wa Mambo ya nje wa nchi za...

error: Content is protected !!