Thursday , 18 April 2024
Home Kitengo Habari Kimataifa Bunge la Congress kufanya maamuzi kwa Trump
Kimataifa

Bunge la Congress kufanya maamuzi kwa Trump

Spread the love

BUNGE la Congress limetaka Urusi iadhibiwe kwa kosa la kuingilia uchaguzi wa rais uliofanyika mwaka jana nchini Marekani, anaandika Catherine Kayombo.

Bunge hilo linatarajia kupiga kura kesho ili kupitisha mswaada huo wa sheria unaopanga kuitaka ofisi ya rais wa Marekani kutoingilia hatua za kidiplomasia zitakazochukuliwa dhidi ya Moscow, mji mkuu wa Urusi.

Kupitishwa kwa sheria hiyo na Bunge la Congress kutamnyima Trump uwezo wa kuondoa kikwazo chochote kitakachopitishwa dhidi ya Urusi.

Aidha, Trump ameunga mkono makubaliano hayo yasiyopendelea upande wowote licha ya kwamba White House ilipinga mswaada huo hapo awali.

Kukataa kupitisha mswaada huo kungeonyesha ushirikiano wa Trump na Urusi katika uchaguzi wa Marekani.

Mswaada huo pia unaruhusu vikwazo dhidi ya Korea Kaskazini, Iran pamoja na Syria. Urusi imeendelea kukataa shutuma za kujihusisha na uchaguzi nchini Marekani na kusisitiza kutokuwa na mamlaka ya kuingilia maamuzi ya kidiplomasia.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Kimataifa

Majaji kuamua hatima ya Zuma leo

Spread the loveMajaji nchini Afrika Kusini leo Jumanne wataamua ikiwa rais wa...

Habari za SiasaKimataifa

Spika Afrika Kusini ajiuzulu kwa tuhuma za rushwa

Spread the loveSpika wa Bunge la Afrika Kusini, Nosiviwe Mapisa-Nqakula ametangaza kujiuzulu...

Habari MchanganyikoKimataifa

Tetemeko la ardhi laua 7, lajeruhi 800 Taiwan

Spread the loveWatu wapatao saba wamefariki dunia na wengine zaidi ya 800...

Habari za SiasaKimataifa

Rais Faye amteua aliyekuwa mfungwa mwenzie kuwa waziri mkuu

Spread the loveRais mpya wa Senegal, Bassirou Diomaye Faye, amemteua Ousmane Sonko...

error: Content is protected !!