Saturday , 3 June 2023
Home Gazeti Habari za Siasa Bunge kutokuwa ‘live’: Spika Ndugai ataja ‘mchawi’
Habari za Siasa

Bunge kutokuwa ‘live’: Spika Ndugai ataja ‘mchawi’

Spread the love

JOB Ndugai, Spika wa Bunge amesema, miongoni mwa sababu za Bunge hilo kutorushwa ‘live’, wabunge wenyewe kutojiheshimu. Anaripoti Dandon Kaijage, Dodoma … (endelea).

Akizungumza bungeni jijini Dodoma leo tarehe 13 Juni 2019, Spika Ndugai amesema kuwa, baadhi ya vitendo vya wabunge hao, vimekuwa vikitia aibu mhimili huo.

“Kuna baadhi ya wabunge ambao wamekuwa wakipiga kelele wakati wa mijadala muhimu kuhusu masilahi ya nchi,” amesema wakati akiwataka wabunge kuwa wasikivu na watulivu wakati Waziri wa Fedha na Mipango, atakapoisoma bajeti mpya ya serikali kwa mwaka wa fedha 2019/20 leo jioni.

“Wengi huwa mnaandika, mnalalamika kwamba kwanini bunge ‘live’ hakuna. Moja ya sababu ni hii hali, ndiyo ukweli wenyewe.

“Unapoonesha ‘live’ hii hali ambayo spika kila wakati anawaambia wabunge tusikilizane, yani nyie wenyewe hamuwezi kusikiliza kila mmoja akaona, ni aibu kubwa,” amesema Spika Ndugai.

Kiongozi huyo wa Bunge amesema, “kwa mfano, hotuba ya leo itasomwa Afrika Mashariki nzima, na hakika mkiweza kuangalia mabunge yote, mtaona utulivu ni tofauti kabisa.

“Kwa wenzetu wanasikiliza, sisi kwetu watu hawana habari, sijui kwa sababu takwimu zinasomwa hapa, unajua si wote wanaweza kuvumilia hesabu.”

Spika Ndugai amewataka wabunge kuwa na desturi ya kuheshimu mijadala ya bunge na kuisikiliza kwa makini, ili waweze kuchangia vyema mijadala hiyo.

“Tuwe na utulivu, watu wanashangaa hili bunge ni la aina gani! watu wanapiga michapo wanageuka nyuma, mwengine anakaa saa nzima anaongea na mwingine, wengine mnawabughuzi wanashindwa kusema ondoka,” amesema Spika Ndugai na kuongeza:

“Serikali inaleta taarifa serious, tuonekane tunaisikiliza taarifa hiyo, nawaombeni tujenge utamaduni wa kusikiliza vitu ili wakati wa kuchangia uchangie kutokana  na taarifa halisi ulizonazo, kuliko unakuja kivyako kwa sababu hujasikiliza.”

Aidha, Spika Ndugai amewaonya wabunge watakaofanya fujo siku ya leo kwamba, atataja majina yao hadharani ili wananchi wao wajue wanachokifanya bungeni.

“Kutembea tembea haipendezi kwa kweli, jioni nitakachofanya nitakua nataja majina tu kwa sababu nina uhakika nchi nzima watakua wanaangalia,” amesema.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

Lusinde: CCM hatuliachii ng’o jimbo la Moshi Mjini

Spread the loveMJUMBE wa Halmashauri Kuu ya Chama cha Mapinduzi (NEC), Livingston...

Habari za SiasaTangulizi

Serikali ya Mapinduzi Zanzibar: Bakharesa hajavamia shamba letu

Spread the love  IKULU Visiwani Zanzibar, imeeleza kuwa eneo la kiwanda cha...

Habari za SiasaTangulizi

Zanzibar watangaza rasmi kuwa shamba la Razaba ni mali yao

Spread the love  SERIKALI ya Mapinduzi Zanzibar (SMZ), imetangaza rasmi kwamba shamba...

Habari za SiasaTangulizi

Rais Mwinyi azindua Kamati ya Maridhiano Visiwani

Spread the love  RAIS wa Serikali ya Mapinduzi Zanzibar (SMZ), Dk. Hussein...

error: Content is protected !!