Wednesday , 27 September 2023
Home Gazeti Habari za Siasa Bunge, Chadema watifuana
Habari za SiasaTangulizi

Bunge, Chadema watifuana

Spread the love

GOGORO kubwa limeibuka kati ya ofisi ya Spika wa Bunge la Jamhuri kwa upande mmoja na familia ya aliyekuwa mbunge wa Buyungu, Mwalimu Kasuku Bilago na Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), kwa upande mwingine. Anaripoti Mwandishi Wetu kutoka Dodoma …  (endelea).

Mgogoro wa sasa umeibuka kufuatia hatua ya ofisi ya Bunge, kuamua kutaka Jumatano wiki hii, kuwa ndiyo siku ya mazishi ya Mwalimu Bilago, kinyume na matakwa ya familia na chama chake.

Kwa mujibu wa makubaliano yaliyofikiwa kati ya familia ya marehemu na uongozi wa Chadema uliongozwa na mwenyekiti wake wa taifa, Freeman Mbowe, mazishi ya mbunge huyo yatafanyika Alhamisi wiki hii.

Lakini Bunge, huku likijua kuwapo kwa makubaliano hayo, lilitangaza kuwa mazishi ya mwanasiasa huyo yatafanyika Jumatano.

Hadi saa tano na nusu usiku wa Jumatatu, pande hizo mbili zilikuwa hazijaweza kukubaliana juu ya siku rasmi ambayo msiba huo utafanyika.

Akizungumza katika mahojiano maalum na gazeti hili, mbunge wa Vunjo (NCCR-Mageuzi), James Mbatia amesema, kinachosababisha kuwapo kwa mvutano huo, ni “Bunge kutotaka kusikiliza wafiwa halisi.”

Mbatia ambaye ni mwenyekiti mwenza wa Umoja wa Katiba ya Wananchi (UKAWA) na abmbaye amekuwa akiwaongoza wabunge wa upinzani bungeni anasema, “ni vizuri jambo hili likapatiwa ufumbuzi wa haraka.”

Habari kamili tutawaletea muda si mrefu

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Kapinga: Usambazaji umeme vijijini mwisho Desemba 2023

Spread the love  NAIBU Waziri wa Nishati, Judith Kapinga, amesema ifikapo mwezi...

Habari za Siasa

Mgongano wa kimasilahi wamhamisha Chande TTTCL

Spread the love  ALIYEKUWA Mkurugenzi Mtendaji wa Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO),...

Habari za SiasaTangulizi

Mgawo wa umeme: Rais Samia ampa miezi sita bosi mpya TANESCO

Spread the love  RAIS Dk. Samia Suluhu Hassan, amempa miezi sita Mkurugenzi...

Habari za Siasa

Rais Samia avunja bodi ya REA

Spread the loveRAIS Dk. Samia Suluhu Hassan, amemteua Balozi Jacob Kingu, kuwa...

error: Content is protected !!