Friday , 29 March 2024
Home Habari Mchanganyiko BRELA watangaza operesheni maalum, kufuta kampuni 5,000
Habari Mchanganyiko

BRELA watangaza operesheni maalum, kufuta kampuni 5,000

Afisa Mtendaji Mkuu wa BRELA, Godfrey Nyaisa
Spread the love

 

WAKALA wa Usajili wa Biashara na Leseni nchini (BRELA), imetangaza kusudio la kufanya operesheni endelevu ya kuzifuta kampuni zinazokiuka sheria, ambapo zaidi ya 5,000 zinatarajiwa kufutwa katika awamu ya kwanza, endapo wamiliki wake hawatathibitisha. Anaripoti Regina Mkonde, Dar es Salaam … (endelea).

Kusudio hilo limetangazwa leo Ijumaa, tarehe 27 Mei 2022 na Afisa Mtendaji Mkuu wa BRELA, Godfrey Nyaisa, akizungumza na wanahabari jijini Dar es Salaam.

Nyaisa amesema, kampuni zitakazofutwa ni zile zilizokiuka Sheria ya Makampuni, ikiwemo kwa kutowasilisha taarifa za mwaka, kushindwa kutimiza malengo kusudiwa ya uanzishwaji wake pamoja na kuelemewa na migogoro baina ya wamiliki.

“Natangaza kusudio la kufuta kampuni 5,676, kama sehemu ya awamu ya kwanza ambayo tunahisi hayafanyi biashara kwa kutimiza matakwa ya kisheria kama nilivuyeleza hapa juu,” amesema Nyaisa.

Mtendaji huyo wa BRELA amesema, wakala unafuta usajili wa kampuni hizo ili ubaki na kampuni zilizo hai, kupunguza majina ya kampuni yasiyofanya kazi na kuzuia kutumika na watu wengine na kupunguza vishoka wanaouza majina hayo.

Aidha, Nyaisa amesema BRELA itatoa notisi ya awamu tatu kwa ajili ya wamiliki kupata fursa ua kuthibitisha iwapo kampuni zao zinafanya kazi.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

Mtandao watetezi wa haki za mazingira Tanzania waundwa

Spread the loveMTANDAO wa watetezi wa haki za mazingira nchini Tanzania, umeundwa...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Kapinga kuongoza usambazaji wa mitungi ya gesi 10,000 ya Taifa Gas

Spread the loveNaibu Waziri wa Nishati, Judith Kapinga ameahidi kuongoza kwa ufanisi...

BiasharaHabari Mchanganyiko

Wafanyabiashara, wawekezaji China waridhia kuwekeza bil. 800 katika sekta 5 nchini

Spread the loveUJUMBE wa wafanyabiashara na wawekezaji wakubwa kutoka Jimbo la Changzhou...

Habari Mchanganyiko

Bil. 4.42 kumaliza uhaba maji kata 2 Musoma Vijijini

Spread the loveWANANCHI wa kata za Busambara na Kiriba, Jimbo la Musoma...

error: Content is protected !!