Wednesday , 24 April 2024
Home Gazeti Habari BREAKING NEWS: Maalim Seif afariki dunia
HabariTangulizi

BREAKING NEWS: Maalim Seif afariki dunia

Spread the love

RAIS wa Zanzibar, Dk. Hussein Mwinyi, ametangaza kifo cha Maalim Seif Sharif Hamad (77), Makamu wa Kwanza wa Rais, Zanzibar, kilichotolea leo Jumatano saa 5:00 asubuhi, katika Hospitali ya Taifa ya Muhimbili jijini Dar es Salaam. Anaripoti Mwandishi Wetu…(endelea)

Rais Mwinyi amesema, Maalim Seif aliyezaliwa tarehe 22 Oktoba 1943 visiwani Pemba, alikuwa akipatiwa matibabu Hospitali ya Muhimbili tangu 9 Februari 2021.

Rais Mwinyi ametangaza siku saba za maombolezo, yatakayoambatana na bendera kupepea nusu mlingoti huku taratibu za mazishi zitatangazwa baadaye kwa ushirikiano na chama chake cha ACT-Wazalendo.

Hadi anafikwa na mauti, Maalim Seif alikuwa Mwenyekiti wa chama cha ACT-Wazalendo.

Endelea kufuatilia MwanaHALISI Online, MwanaHALISI TV na mitandao yetu ya kijamii kwa habari na taarifa mbalimbali

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaTangulizi

Biteko ataja vipaumbele 7 bajeti nishati 2024/25

Spread the love  NAIBU Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Dk. Doto...

Habari za SiasaTangulizi

Mpwa wa Magufuli mbaroni kwa kusambaza picha za utupu

Spread the loveJESHI la Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam limewakamata...

Habari za SiasaTangulizi

Shibuda amlima waraka mzito Bulembo

Spread the loveMKONGWE wa siasa nchini, John Shibuda amemshukia kada maarufu wa...

Habari za SiasaTangulizi

Rais Samia ataja mikakati ya kufikia trilioni 2 biashara Uturuki, Tz

Spread the loveWakati Tanzania na Uturuki zikidhamiria kuongeza kiwango cha biashara hadi...

error: Content is protected !!