MAALIM Seif Sharif Hamad, mshauri mkuu wa Chama cha ACT-Wazalendo, amekamatwa na Jeshi la Polisi visiwani Zanzibar. Anaandika Kelvin Mwaipungu, Zanzibar … (endelea).
Kiongozi huyo ambaye aliwahi kuwa Makamu wa Pili wa Rais katika Serikali ya Mapinduzi Zanzibar (SMZ), amekamatwa leo tarehe 31 Julai 2019 akiwa kwenye Kongamano la Kuadhimisha Miaka 9 ya Maridhiano visiwani humo.
Kongamano hilo lilisimamishwa saa 6 mchana kwa agizo la Jeshi la Polisi visiwani humo baada ya mada iliyokuwa ikiwasilishwa na Maalim Seif.
Habari zaidi zitakujia….
Leave a comment