Friday , 29 March 2024
Home Habari Mchanganyiko BoT yakumbushwa kudhibiti fedha haramu
Habari Mchanganyiko

BoT yakumbushwa kudhibiti fedha haramu

Benki Kuu ya Tanzania
Spread the love

BENKI Kuu ya Tanzania (BoT), imetakiwa kufuata muongozo wa fedha unaokubalika ili kudhibiti fedha haramu zisiingie katika mzunguko halali, anaandika Mwandishi Wetu.

Aidha, kupitia muongozo huo BoT itafahamu fedha zinazoingizwa nchini na kufahamu zinaingia kwa njia gani.

Kauli hiyo imetolewa na Waziri wa Fedha na Mipango wa Zanzibar, Dk. Khalid Salum Mohammed wakati akifungua kikao cha siku tano cha taasisi ya kudhibiti utakasishaji wa fedha haramu kwa nchi za Mashariki na Kusini mwa Afrika uliofanyika visiwani Zanzibar.

“Upo muuongozo wa fedha ambao umekubalika katika kupambana na utakatisishaji wa fedha haramu kwa hivyo BoT inatakiwa kufuatilia hatua kwa hatua utekelezaji wake,” amesema.

Aidha, Dk. Mohammed alishauri kwamba ni vyema mabenki kujuwa wateja wao na kuzifahamu kazi zao kabla ya kuingiza fedha katika benki ili kuweza kuzitambuwa kama fedha haramu au halali.

Amesema awali walikuwa wakikabiliwa na changamoto ya kutunga sheria za kimataifa za kupambana na fedha haramu kwa nchi moja moja na kwamba hivi sasa wanatumia sheria zinazofanana.

Amesema fedha haramu zinazotokana na biashara za dawa za kulevya na usafirishaji wa binadamu hutumika kufadhili shughuli za kigaidi hivyo kuna umuhimu mkubwa kwa taasisi za kifedha kudhibiti masuala hayo.

Ameongeza kuwa fedha hizo huko zinakotoka huwa hazitumiki na kwamba husafirishwa na kuletwa Afrika au Tanzania ili kuwekezwa katika mahoteli na baadaye kurudi katika nchi zilizotoka fedha hizo na kuonekana ni fedha halali.

“Biashara hii inaweza kusababisha Benki kufa na uchumi unaweza kuathirika kwa sababu wakati mwIngine fedha hizi zinakuja kwa wingi na zinaweza kuwafukuza wawekezaji hivyo ni muhimu kuwa na nguvu za pamoja ili kuondokana na tatizo hili,” alisema.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

DAWASA waanza utekelezaji agizo la Samia

Spread the loveMamlaka ya Majisafi na Usafi wa Mazingira Dar es Salaam...

Habari MchanganyikoKimataifa

Zuma akataliwa kugombea urais

Spread the loveTUME Huru ya Uchaguzi Afrika Kusini (IEC) imemwondoa rais wa...

Habari Mchanganyiko

Mtandao watetezi wa haki za mazingira Tanzania waundwa

Spread the loveMTANDAO wa watetezi wa haki za mazingira nchini Tanzania, umeundwa...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Kapinga kuongoza usambazaji wa mitungi ya gesi 10,000 ya Taifa Gas

Spread the loveNaibu Waziri wa Nishati, Judith Kapinga ameahidi kuongoza kwa ufanisi...

error: Content is protected !!