Friday , 29 September 2023
Home Habari Mchanganyiko BOT yailima DTB benki faini Bil. 1
Habari Mchanganyiko

BOT yailima DTB benki faini Bil. 1

Spread the love

BENKI ya Diamond Trust (DTB) imepigwa faini ya kiasi cha Sh. 1 Bilioni na Benki Kuu ya Tanzania (BOT) kwa kukaidi agizo la kuanzisha kituo cha taarifa hapa nchini. Anaripoti Regina Mkonde … (endelea).

Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na BOT jana tarehe 12 Julai 2019, inaeleza kwamba, ilitoa maagizo kwa benki na taasisi zote za fedha zinazofanya shughuli zake hapa nchini, kuanzisha vituo vya taarifa ‘Data Centre’, lakini DTB haikutekeleza agizo hilo.

Sehemu ya taarifa  hiyo inaeleza kuwa, BOT ilitoa barua mnamo tarehe 3 Machi 2014 na 29 February 2016 kwa ajili ya kuzielekeza benki za taasisi za fedha nchini, kuanzisha vituo hivyo kwa lengo la kuhakikisha taarifa na huduma za sekta hiyo, zinapatikana wakati wote.

“…DTB haikutekeleza maagizo, licha ya kuthibitisha kwamba imekwisha anzisha kituo cha taarifa,” inaeleza sehemu ya taarifa ya BOT .

Aidha, taarifa ya BOT imeongeza kuwa, DTB itatozwa riba ya asilimia kumi kwa kila mwezi, endapo itashindwa kulipa faini kwa muda husika.

BOT imezitaka benki na taasisi za fedha zinazofanya shughuli zake hapa nchini kuanzisha vituo vya taarifa.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

Vijana 400 waguswa na programu ya “Learning for Life” ya SBL

Spread the love  PROGRAMU ya “Learning for Life” imetimiza dhamira ya Serengeti...

BiasharaHabari Mchanganyiko

Stamico yafungua fursa za kiuchumi kwa makundi maalumu

Spread the loveSHIRIKA la Madini la Taifa (STAMICO) limemwaga neema kwa watu...

BiasharaHabari Mchanganyiko

Maabara ya bilioni 5 upimaji madini yazinduliwa Geita, inapima kwa mionzi

Spread the loveZaidi ya Sh bilioni tano zimewekezwa katika kampuni ya MSALABS...

ElimuHabari Mchanganyiko

Wanafunzi Nyamkumbu wanolewa na GGML kuhusu taaluma ya madini

Spread the loveZAIDI ya Wanafunzi 50 kutoka Shule ya Sekondari ya Wasichana...

error: Content is protected !!