Friday , 29 September 2023
Home Kitengo Maisha Elimu Bosi ya Mikopo yafungua dirisha la rufaa
Elimu

Bosi ya Mikopo yafungua dirisha la rufaa

Bodi ya Mikopo Elimu ya Juu
Spread the love

BODI ya Mikopo ya Wanafunzi wa Elimu ya Juu (HESLB) leo tarehe 21 Novemba 2018 imeanza kupokea rufaa za mikopo kwa mwaka wa masomo wa 2018/19 kwa njia ya mtandao. Anaripoti Regina Mkonde … (endelea).

Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa leo na HESLB, inaeleza kuwa, dirisha la kuwasilisha rufaa hizo liko wazi kwa muda wa siku tano hadi Novemba 25 mwaka huu, ambapo wanafunzi wenye malalamiko wanatakiwa kutumia fursa hiyo.

“HESLB imefungua dirisha hili ili kutoa fursa kwa wanafunzi wahitaji ambao hadi sasa hawajapa mkopo au hawajaridhika na kiwango cha mkopo walichopangiwa, kuwasilisha maelezo na nyaraka kuthibitisha uhitaji wao,” inaeleza sehemu ya taarifa hiyo.

Taarifa hiyo imeongeza kuwa, baada ya rufaa hizo kuwasilishwa na kupitiwa, wanafunzi watakaobainika kutimiza masharti na sifa watapangiwa mikopo kabla ya mwisho wa mwezi huu wa Novemba.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Elimu

Wazazi wa wanafunzi waliokosa nafasi vyuo vikuu waonyeshwa njia na GEL

Spread the loveWAKALA wa Elimu ya Vyuo Vikuu Nje ya Nchi, Global Education...

ElimuHabari Mchanganyiko

Wanafunzi Nyamkumbu wanolewa na GGML kuhusu taaluma ya madini

Spread the loveZAIDI ya Wanafunzi 50 kutoka Shule ya Sekondari ya Wasichana...

Elimu

Green Acres kuwakatia bima wanafunzi wote

Spread the loveShule ya Green Acres imejipanga kufanya mambo makubwa kwa mwaka...

Elimu

Vipaji Green Acres vyawafurahisha wazazi

Spread the love WANAFUNZI wa Shule ya Msingi Green Acres, wamewapagawisha wazazi...

error: Content is protected !!