Wednesday , 24 April 2024
Home Habari Mchanganyiko Bosi KADCO afariki dunia
Habari Mchanganyiko

Bosi KADCO afariki dunia

Mhandisi Christopher Mukoma, Kaimu Mkurugenzi wa Kampuni ya Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Kilimanjaro (KADCO)
Spread the love

MHANDISI Christopher Mukoma, Kaimu Mkurugenzi wa Kampuni ya Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Kilimanjaro (KADCO), amefariki dunia leo Ijumaa tarehe 8 Mei 2020, kutokana na tatizo la shinikizo la damu. Anaripoti Regina Mkonde, Dar es Salaam … (endelea).

Taarifa hiyo imetolewa leo na Julius Nyamkama, Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Viwanja vya Ndege Tanzania (TAA), wakati akizungumza na MwanaHALISI ONLINE kwa simu.

Nyamkama amesema Mhandisi Mukoma alifariki dunia akiwa nyumbani kwake mkoani Arusha, baada ya kusumbuliwa na shinikizo la damu.

Amesema marehemu alianza kusumbuliwa na tatizo hilo siku mbili zilizopita.

“Ni kweli Mhandisi Mukoma amefariki dunia leo akiwa nyumbani kwake Arusha. Alikuwa anasumbuliwa na tatizo la shinikizo la damu na alianza kuumwa siku mbili zilizopita,” amesema Nyamkama.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

THRDC yaongeza mkataba wa ushirikiano na ABA

Spread the love  MTANDAO wa Watetezi wa Haki za Binadamu Tanzania (THRDC),...

Habari Mchanganyiko

Rufaa ya Equity Benki, State Oil yakwama

Spread the loveMAHAKAMA ya Rufani, jijini Dar es Salaam, imeshindwa kuendelea na...

Habari Mchanganyiko

Bodaboda waeleza mafanikio mafunzo usalama barabarani

Spread the loveMADEREVA bodaboda katika Jiji la Dodoma wameeleza jinsi mafunzo ya...

BiasharaHabari Mchanganyiko

NBC yaahidi kuendelea kuunga mkono Serikali za Mitaa

Spread the loveBenki ya Taifa ya Biashara (NBC) imesisitiza dhamira yake ya...

error: Content is protected !!