Friday , 29 March 2024
Home Kitengo Habari Kimataifa Bosco Ntaganda akutwa na hatia
Kimataifa

Bosco Ntaganda akutwa na hatia

Bosco Ntaganda
Spread the love

MAHAKAMA ya Kimataifa ya Makosa ya Jinai (ICC), imemtia hatiani kwa makosa ya uhalifu wa kivita na binadamu Bosco Ntaganda,  kiongozi wa zamani wa waasi nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo (DRC). Inaripoti Mitandao ya Kimataifa … (endelea).

Majaji wa ICC wamemkuta na hatia Ntaganda kwa makosa 18 ya uhalifu wa kivita na uhalifu dhidi ya binadamu, uliotokea katika Mji wa Mashariki wa Ituri mwaka 2002 na 2003.

Robert Fremr, Jaji wa ICC amesema, Ntaganda anatuhumiwa kutoa amri zenye lengo la kuuwa na kutesa raia wasio na hatia, alipokuwa kiongozi wa waasi.

Makosa mengine yaliyotajwa na waendesha mashtaka hao ni pamoja na kuhusishwa na vitendo vya ubakaji na utumwa wa ngono, kumuuwa kasisi wa kikatoliki pamoja na kuwasajili watoto kwenye jeshi wakiwemo wasichana.

Vile vile, Ntaganda anatuhumiwa kuongoza operesheni ya waasi wa Union of Congolese Patriots (UCP).

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari MchanganyikoKimataifa

Zuma akataliwa kugombea urais

Spread the loveTUME Huru ya Uchaguzi Afrika Kusini (IEC) imemwondoa rais wa...

KimataifaTangulizi

Zuma akataliwa kugombea urais

Spread the love  TUME Huru ya Uchaguzi Afrika Kusini (IEC) imemwondoa rais...

Habari za SiasaKimataifa

Mwanaye rais jela miaka miaka 6 kwa dawa za kulevya

Spread the loveMwanawe rais wa zamani wa Guinea-Bissau amehukumiwa kifungo cha miaka...

Habari za SiasaKimataifa

Faye aahidi kuongoza kwa unyenyekevu, wagombea wenzie wakubali yaishe

Spread the loveMgombea wa upinzani Senegal, Bassirou Diomaye Faye anajiandaa kuwa rais...

error: Content is protected !!