Saturday , 20 April 2024
Home Gazeti Habari Bodi ya mazao, NFRA zamwagiwa mabilioni kununua mahindi ya wakulima
Habari

Bodi ya mazao, NFRA zamwagiwa mabilioni kununua mahindi ya wakulima

Spread the love

 

MKURUGENZI wa Idara ya Habari Maelezo na Msemaji Mkuu wa Serikali, Gerson Msigwa amesema Serikali imeidhamini Bodi ya Mazao Mchanganyiko kupatiwa mkopo wa Sh.50 bilioni nyingine ili kwenda kununua mahindi kwa wakulima na kuyauza nje. Anaripoti Gabriel Mushi (endelea..)

Pia, amesema tayari serikali imetoa Sh.50 bilioni kwa Wakala wa Taifa wa Hifadhi ya Chakula (NFRA), kwa ajili ya kununua mahindi mbali na Sh bilioni 14 za awali ilizopatiwa.

Msigwa ametoa kauli hiyo leo Jumapili tarehe 12 Septemba 2021 jijini Dodoma wakati akizungumza na waandishi wa habari pamoja na Watanzania kama ulivyoutaratibu wake wa kila wiki.

Msigwa amesema mbali na NFRA ambao wananunua mahindi kwa ajili ya usalama wa nchi, Bodi ya Nafaka na Mazao Mchanganyiko Tanzania (CPB), ambayo inanunua mahindi kwa ajili ya biashara imepata soko la tani 100,000 nchini Kenya, tani 200,000 Sudani Kusini na tani 200,000 Shirika la Chakula duniani.

“Wakati wafanyabiashara wakinunua kilo moja ya mahindi kati ya Sh 250 hadi Sh.350 kwa kilo moja, Wakala wa Taifa wa Hifadhi ya Chakula (NFRA) itanunua Sh.500 kwa kilo ilihali Bodi ya Nafaka na Mazao Mchanganyiko Tanzania (CPB) itanunua kwa bei ya juu zaidi ili kumnufaisha mkulima,” amesema

“Mahindi yamezalishwa tani milioni saba wakati Tanzania matumizi yake ni tani 500,000, kwa hiyo uzalishaji ni mzuri, umekwenda mara mbili ya uzalishaji wa msimu uliopita,” amesema.

Pia, amesema bei ya mbolea imepanda kutokana na athari za Corona lakini serikali imeondoa vikwazo vyote ili kila mtu alete mbolea huku Serikali kupitia wakala wake wakihakikisha ubora.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

HabariSiasa

Dk. Rose Rwakatare atoa kadi 500 kila Wilaya Morogoro

Spread the loveMWENYEKITI wa Jumuiya ya Wazazi CCM Mkoa wa Morogoro, Dk...

ElimuHabari

CBE, WMA wasaini makubaliano wanafunzi kusoma wakifanyakazi

Spread the loveNAIBU Spika Musa Azzan Zungu amekipongeza Chuo cha Elimu ya...

HabariTangulizi

Dk. Slaa, Mwabukusi kuhojiwa na jeshi la Polisi Mbeya

Spread the loveJESHI la Polisi jijini Mbeya, linawashikilia kwa mahojiano Dk. Wilbroad...

HabariHabari Mchanganyiko

Kairuki Hospital Green IVF  yawanoa madaktari kuhusu upandikizaji mimba

Spread the love KITUO cha Upandikizaji Mimba cha Kairuki Hospital Green IVF...

error: Content is protected !!