MARA baada ya kumalizika kwa mchezo wa Ligi Kuu Tanzania Bara kati ya Mtibwa Sugar dhidi ya Yanga, Bodi ya Ligi imepiga marufuku kutumika kwa Uwanja wa Jamhuri uliopo mkoani Morogoro kutumika katika michezo yote ya kimashindano. Anaripoti Kelvin Mwaipungu, Morogoro … (endelea).
Bodi ya Ligi imewataka wahusika wa uwanja huo kufanya marekebisho katika eneo la kuchezea (pitch), vyumba vya kubadilishia nguo na sehemu za kukaa wachezaji wa akiba.
Kiwanja hicho ambacho leo kimechezwa mchezo wa ligi na kushuhudia Yanga ikiibuka na pointi tatu kwa ushindi wa bao 1-0.
Mpaka sasa bodi hiyo imefungia jumla ya viwanja vimne kutumika katika michezo ya kimashindano ambavyo ni Ushirika Moshi, Mabatini Pwani, Highland Estates uliokuwa ukitumiwa na Klabu ya Ihefu uliopo Mbalizi, Mbeya na Uwanja wa Gwambina
Leave a comment