Thursday , 28 March 2024
Home Kitengo Michezo Bocco nae asalia Simba, asaini mkataba mpya
MichezoTangulizi

Bocco nae asalia Simba, asaini mkataba mpya

Spread the love

 

UONGOZI wa klabu ya Simba umemalizana na nahodha wa kikosi hiko John Bocco kwa kumsainisha mkataba mpya mara baada yaw a awali kumaliza mwisho wa msimu wa 2020/21. Anaripotio Kelvin Mwaipungu..

Dakika chache mara baada ya kumsainisha beki wa kushoto Mohammed Hussein, kupitia ukurasa wa Instagram wa klabu hiyo uliweka picha ilionesha nahodha huyo akisaini mkataba mpya kuendelea kukipiga klabuni hapo.

Licha ya kuweka picha hiyo lakini bado haijajulikana Bocco amesaini mkataba wa muda gani na thamani yake haikuwa wazi.

Nahodha huyo kwa sasa kwenye Ligi Kuu Tanzania Bara amepachika jumla ya mabao 10 na kutoa pasi mbili za mabao (assist) na kuwa amehusika katika mabao 12 kati ya 58 yaliyofungwa na klabu hiyo mpaka sasa.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaTangulizi

Mashirika matano yapata hasara mabilioni ya fedha

Spread the loveMASHIRIKA matano ya Serikali yanayojiendesha kibiashara, yamepata hasara ya mabilioni...

Habari za SiasaTangulizi

CAG aibua madudu halmashauri 10, TANESCO na MSD

Spread the loveRIPOTI ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali...

Habari za SiasaTangulizi

Deni la Serikali laongezeka kwa trilioni 11

Spread the loveDENI la Serikali imeongezeka kwa takribani Sh. 11 trilioni sawa...

Habari za SiasaTangulizi

Mapya yaibuka wamasai waliohamishwa Ngorongoro kwenda Msomera

Spread the loveMAPYA yameibuka kuhusu zoezi la Serikali kuwahamisha kwa hiari wamasai...

error: Content is protected !!