Saturday , 25 March 2023
Home Gazeti Habari za Siasa Bilioni 8.4 zatengwa ujenzi mifereji ya maji Mbweni
Habari za Siasa

Bilioni 8.4 zatengwa ujenzi mifereji ya maji Mbweni

David Silinde, Naibu Waziri wa Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI)
Spread the love

 

SERIKALI ya Tanzania, imetenga Sh.8.4 bilioni kwa ajili ya ujenzi wa mirefeji ya maji katika maeneo ya Mbweni mkoani Dar es Salaam. Anaripoti Nasra Bakari, DMC … (endelea).

Hilo limesemwa leo Jumanne, tarehe 27 Aprili 2021, bungeni jijini Dodoma na Naibu Waziri wa Tamisemi, David Silinde wakati akijibu swali la Felista Njau, Mbunge wa Viti Maalum (asiye na chama), baada ya kufukuzwa Chadema yeye pamoja na wenzake 18 akiwemo Halima Mdee.

“Je, serikali ina mkakati gani wa kutatua tatizo la mafuriko katika maeneo Mbweni, Teta, Bunju Basihaya, Kunduchi, Nyamachabes, Ununio na Mikocheni katika jimbo la Kawe,” ameuliza Njau

Akijibu swali hilo, Silinde amesema, serikali inafanya tathmini ili kuhakikisha inasaidia maeneo yote ambayo yanakubwa na mafuriko hususani jimbo la Kawe.

Halima Mdee

“Serikali ipo kazini katika kufanya tathmini ya mwisho ili kusaidia maeneo ya Mbweta, Teta, Bunju Basihaya, Kunduchi, Nyamachabes, Ununio na Mikocheni kupunguza tatizo la mafuriko katika jimbo hilo la kawe,” alisema Silinde.

Katika swali la nyongeza la Njau, ameuliza ni lini serikali itaweka mikakati madhubuti kuondoa majanga ya mafuriko hususani kwa kujenga mifereji?

Silinde amejibu swali hilo akisema, moja ya mkakati wa serikali ni kila barabara itakayojegwa kwa sasa, itaambatanishwa na ujenzi wa miundombinu ambayo ni mifereji.

“Serikali imetenga Sh.8.4 bilioni kwa ajili ya ujenzi wa mfereji wa maji ya mvua yenye urefu wa kilomita 8.89, katika Kata ya Mbweni na awamu nyingine itajumuisha maeneo mengine yaliyobaki,” alisema Silinde ambaye ni Mbunge wa Tunduma (CCM).

“Vilevile wataendelea kujenga na kukarabati miundombinu ya barabara, madaraja na mifereji ya maji ya mvua ili kuondoa kero ya mafuriko maeneo mbalimbali jijini Dar es Salaam ikiwemo jimbo la Kawe,” alisema Silinde.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

Rais Samia aagiza iundwe kamati ya pamoja ya Mawaziri mradi wa BBT

Spread the love  RAIS Dk. Samia Suluhu Hassan, amewaagiza mawaziri kuunda kamati...

Habari za Siasa

Rais Samia apangua makatibu tawala mikoa, ateua Kamishna DCEA

Spread the loveALIYEKUWA Kamishna wa Mamlaka ya Kudhibiti Dawa za Kulevya, Gerald...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

M/kiti bodi ya wadhamini Chadema afariki dunia

Spread the loveMWENYEKITI wa Bodi ya Wadhamini ya Chama cha Demokrasia na...

Habari za Siasa

Zitto: Nikifa Ado atavaa viatu vyangu

Spread the love  KIONGOZI Mkuu wa Chama cha ACT Wazalendo, Zitto Kabwe...

error: Content is protected !!