Thursday , 25 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Bilioni 63 zakusanywa tozo miamala ya simu
Habari za Siasa

Bilioni 63 zakusanywa tozo miamala ya simu

Dk. Mwigulu Nchemba, Waziri wa Fedha na Mipango
Spread the love

 

SERIKALI imesema tangu tozo za miamala ya simu ianze kukusanywa tayari zimepatikana Sh. 63 bilioni hadi kufiki tarehe 30 Agosti, mwaka huu. Anaripoti Mwandishi Wetu, Dodoma … (endelea).

Pia fedha hizo tayari zimeshapelekwa kufanya kazi ambapo jumla ya vituo vya afya 220 vimeanza kujengwa katika tarafa zote zisizokuwa na vituo vya afya nchini.

Taarifa hiyo imetolewa na Waziri wa Fedha na Mipango, Dk. Mwigulu Nchemba leo tarehe 1 Septemba 2021 wakati akizungumza na waandishi wa habari kutoa ufafanuzi kuhusu tozo mbalimbali zilizoanzishwa na Serikali.

Amesema hakuna tarafa yoyote nchi nzima ambayo haitakuwa na kituo cha afya kwasasa.

“Kodi yetu imeleta matokeo, Watanzania tutembee kifua mbele kwa kujenga nchi yetu wenyewe,” amesema.

Pia amesema watu milioni 30 wanaofanya miamala ya Sh 1 hadi Sh 999 kwa siku  hawakukatwa tozo ya kutuma na kutoa fedha.

“Tumeachia miamala zaidi ya milioni 29 kwa watu ambao wanatumiana kuanzia shilingi moja mpaka Sh999, watu wanaotumiana viwango vile tuliiachilia yote ile kwa sababu dira ya rais sio kukusanya hela tu anaangalia na ustawi wa jamii,  amesema.

1 Comment

  • Ndugu Mwigulu,
    Kwanini tozo za miamala haziendi kujenga viwanda mama vya kuyeyushia vyuma, kutenganisha vyuma na tintanium, vanadium, na elementi nyingine?
    Kwanini uchimbaji wa mashimo wazi ya dhahabu, gesi, Helium na almasi yasifanywe na serikali kwanza kabla ya kuingia Dar-es-salaam Stock Exchange (DSE) watanzania wanunue hisa?
    Kwanini DSE haina 80% ya makampuni yote makubwa nchini kama ilivyo ulaya na kwingineko.
    Huko ndiko mtaji na wazawa watapatikana….karne hii ya 21.

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

Kilosa yawa mfano wa kuigwa miradi ya Mwenge nchini

Spread the love  KIONGOZI wa Mbio za Mwenge Kitaifa Godfrey Mzava amezitaka...

Habari za SiasaTangulizi

Biteko ataja vipaumbele 7 bajeti nishati 2024/25

Spread the love  NAIBU Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Dk. Doto...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Mwekezaji amwaga bil. 39 kujenga viwanda 3 vya uchenjuaji

Spread the loveKampuni ya Mineral Access System Limited (MAST) inayoiwakilishwa kampuni ya...

Habari za SiasaTangulizi

Mpwa wa Magufuli mbaroni kwa kusambaza picha za utupu

Spread the loveJESHI la Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam limewakamata...

error: Content is protected !!