HALMASHAURI ya mji Tunduma iliyopo wilayani Momba mkoani Songwe imepatiwa Sh 17 bilioni kutoka serikali kuu kujenga bandari kavu katika mtaa wa Mpemba. Anaripoti Ibrahim Yassin, Songwe …(endelea).
Bandari hiyo inatajwa kuwa itachochea mapato kwa halmashauri na serikali kwa ujumla pamoja na kupunguza msongamano kwenye mpakani wa Tunduma na Nakonde.
Inaelezwa kuwa asilimia 72 ya mizigo inayovushwa kwenye Bandari ya Dar Es salaam kuelekea mpakani Tunduma.
Akizungumza mwishoni mwa wiki, Mkurugenzi mtendaji wa halmashauri hiyo, Philimon Magesa alisema Tunduma ni mji wa kibiashara ambao umekuwa ukielemewa na uwingi wa magari yanayovusha mizigo kwenda kwenye nchi wanachama wa Jumuiya ya kusini mwa Afrika (SADC) hivyo mikakati ya ujenzi wa Bandari kavu utaongeza mapato kwa Serikali.
Alisema nia ya ujenzi wa Bandari hiyo ni kutanua wigo wa utoaji huduma kwa jamii zote hali itakayoongeza uchumi wa nchi.
Mjumbe wa kamati tendaji kutoka chama cha madereva Tanzania, Mussa Samwel alisema yeye na wenzake kwenye umoja huo wamepata taarifa kuhusu ujenzi wa Bandari hiyo na kusema kuwa kutokana na umuhimu wake ipo haja serikali kuharakisha ujenzi huo na kutatua changamoto zilizopo za kimpaka ziweze kutatuliwa.
Leave a comment