Tuesday , 23 April 2024
Home Habari Mchanganyiko Bilioni 17 kujenga bandari kavu Tunduma
Habari Mchanganyiko

Bilioni 17 kujenga bandari kavu Tunduma

Spread the love

HALMASHAURI ya mji Tunduma iliyopo wilayani  Momba mkoani Songwe imepatiwa Sh 17 bilioni kutoka serikali kuu kujenga bandari kavu katika mtaa wa Mpemba. Anaripoti Ibrahim Yassin, Songwe …(endelea).
Bandari hiyo inatajwa kuwa itachochea mapato kwa halmashauri na serikali kwa ujumla pamoja na kupunguza msongamano kwenye mpakani wa Tunduma na Nakonde.

Inaelezwa kuwa asilimia 72 ya mizigo inayovushwa kwenye Bandari ya Dar Es salaam kuelekea mpakani Tunduma.

Akizungumza mwishoni mwa wiki, Mkurugenzi mtendaji wa halmashauri hiyo, Philimon Magesa alisema Tunduma ni mji wa kibiashara ambao umekuwa ukielemewa na uwingi wa  magari yanayovusha mizigo kwenda kwenye nchi wanachama wa Jumuiya ya kusini mwa Afrika (SADC) hivyo mikakati ya ujenzi wa Bandari kavu utaongeza mapato kwa Serikali.

Alisema nia ya ujenzi wa Bandari hiyo ni kutanua wigo wa utoaji huduma kwa jamii zote hali itakayoongeza uchumi wa nchi.

Mjumbe wa kamati tendaji kutoka chama cha madereva Tanzania, Mussa Samwel alisema yeye na wenzake kwenye umoja huo wamepata taarifa kuhusu ujenzi wa Bandari hiyo na  kusema kuwa kutokana na umuhimu wake ipo haja serikali kuharakisha ujenzi huo na kutatua changamoto zilizopo za kimpaka ziweze kutatuliwa.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

NMB yadhamini Mkutano Mkuu ALAT, kufunguliwa na Samia

Spread the loveBENKI ya NMB, imekabidhi hundi yenye thamani ya Sh. 120...

Habari Mchanganyiko

DC ampongeza Dk. Rose Rwakatare kwa kusaidia waathirika wa mafuriko Mlimba

Spread the loveMWENYEKITI wa Wazazi CCM Mkoa wa Morogoro, Dk.  Rose Rwakatare...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Mipango na uwekezaji kutumia bilioni 121.3, mradi wa Bagamoyo wapewa kipaumbele

Spread the loveWIZARA ya Ofisi ya Rais, Mipango na Uwekezaji, imeliomba Bunge...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Mbunge ataka kasi uzalishaji walimu ipunguzwe akidai hakuna ajira

Spread the loveMBUNGE wa Mlalo (CCM), Rashid Shangazi, ameishauri Serikali ipunguze kasi...

error: Content is protected !!