Friday , 29 March 2024
Home Kitengo Michezo Bilionea Uganda ajitosa kuinunua Chelsea
Michezo

Bilionea Uganda ajitosa kuinunua Chelsea

Joel Jaffer A’ita
Spread the love

 

BILIONEA Joel Jaffer A’ita raia wa Uganda ameibua gumzo baada ya kuwasilisha ombi la kutaka kuinunua Klabu ya Soka ya Chelsea inayoshiriki Ligi Kuu ya England. Anaripoti Mwandishi Wetu … (endelea).

Bilionea huyo ambaye ni Mhandisi wa ujenzi kitaaluma ambaye ana Shahada ya Kwanza kutoka Chuo Kikuu cha Makerere, pia anamiliki Klabu ya Michezo ya Arua Hill ya Ligi Kuu ya Uganda.

Aliwasilisha rasmi ombi lake la kuinunua The Blues, na kuwa raia wa pili wa Uganda kutoa zabuni kwa klabu ya soka ya Uingereza baada ya jaribio la Michael Ezra Mulyoowa kufanya hivyo kwa Leeds United mwaka 2004.

“Niko tayari kutwaa Klabu ya Soka ya Chelsea ” A’ita aliiambia Kawowo Sports Media Alhamisi.

A’ita ametoa ofa ya dola bilioni 3.3 kwa bilionea wa Urusi, Roman Abramovich ambaye ni mmiliki wa Klabu hiyo ya Chelsea na anakusudia kuita klabu hiyo ‘Klabu ya Soka ya Kongolo (Kongolo FC)’

“Kufuatia taarifa kwa umma kuhusu nia ya Chelsea FC kuuzwa, ningependa kueleza nia yetu ya kununua klabu. Kwa sasa klabu hiyo ina thamani dola za Marekani 3.2 bilioni (Tsh trilioni 7.4) tutatoa dola bilioni 3.3 (Tsh trilioni 7.6). Tunakusudia kubadili jina la klabu kama Kongolo FC,” Aita aliandika katika barua hiyo kwa Abramovich.

Aita aliingia katika ulingo wa soka nchini Uganda mwaka wa 2019 alipotwaa Klabu ya Soka ya Doves All Stars.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Makala & UchambuziMichezo

TFF kuamua hatima ya Amrouche

Spread the loveHATIMA ya Kocha Mkuu wa Taifa Stars, Adel Amrouche kuendelea...

Habari za SiasaMichezo

Matinyi: Dk. Ndumbaro alifanya utani ukaguzi mechi za Yanga, Simba

Spread the loveMsemaji Mkuu wa Serikali, Mobhare Matinyi amesema kauli iliyotolewa na...

Michezo

Gethsemane Group Kinondoni (GGK) waachia video ya Bwana Wastahili

Spread the loveWAIMBAJI maarufu nchini kutoka Gethsemane Group Kinondoni (GGK)SDA wameachia video...

BiasharaMichezo

Gamondi kocha bora mwezi Februari, NBC yamjaza manoti

Spread the loveBenki ya Taifa ya Biashara (NBC) ambae ni mdhamini Mkuu...

error: Content is protected !!