Friday , 19 April 2024
Home Habari Mchanganyiko Bila kusafiri hupati Paspoti – Uhamiaji
Habari MchanganyikoTangulizi

Bila kusafiri hupati Paspoti – Uhamiaji

Spread the love

IDARA ya Uhamiaji nchini Tanzania imeeleza, ili mtu yeyote aweze kupewa hati ya kusafiria (paspoti), ni lazima awe na kusudio la kusafiri. Anaandika Mwandishi Wetu, Dar es Salaam…(endelea).

Kauli hiyo imetolewa leo Jumanne tarehe 16 Machi 2021 na Paul Mselle, Msemaji wa Idara ya Uhamiaji alipozungumza na chombo kimoja cha habari nchini.

Amesema, hati ya kusafiria ni tofauti na vitambulisho vingine vya kawaida, na kwamba hati hiyo ni mali ya serikali.

“…ni lazima awe na dhumuni la kusafiri, kama hana safari hatuwezi kumapatia pasi hiyo,” amesisitiza Mselle.

Ofisa huyo amesema, ni marufuku kwa mtu yeyote kutumia hati hiyo kwa nia ovu, na kwamba kwa kuwa ni mali ya serikali, ikitumika vibaya muhusika anaweza kupokwa.

1 Comment

  • Siku hizi ukitaka kununua tiketi ya ndege unaulizwa namba ya pasipoti, Halikadhalika ukiomba visa au nafasi ya masomo.. Je wakuu wa uhamiaji wanaelewa hilo?
    Ajabu wao wanasema kwanza fanya maandalizi ya safari kisha omba pasipoti

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

BiasharaHabari Mchanganyiko

NMB Pesa Akaunti yawavutia wakaguzi wa ndani Afrika

Spread the loveUbunifu wa bidhaa bora wa Benki ya NMB pamoja na...

KimataifaTangulizi

Mkuu wa majeshi Kenya afariki, Ruto atangaza maombolezo

Spread the loveRais wa Kenya, William Ruto ametangaza maombezo ya siku tatu...

Habari za SiasaTangulizi

Tanzania, Uturuki zanuia kukuza biashara, uwekezaji

Spread the loveSERIKALI za Tanzania na Uturuki zimekubaliana kuendeleza dhamira ya kuimarisha...

Habari Mchanganyiko

Carbon First, Ruangwa wasaini makubaliano ya biashara ya hewa ukaa

Spread the love  KAMPUNI ya Carbon First Tanzania Limited na Halmashauri ya...

error: Content is protected !!