Saturday , 25 March 2023
Home Gazeti Habari Mchanganyiko Bil. 40 kupunguza uhaba wa mbegu
Habari Mchanganyiko

Bil. 40 kupunguza uhaba wa mbegu

Baadhi ya mifuko ya mbegu bora za kisasa
Spread the love

 

SERIKALI ya Tanzania, imepanga kutumia Sh. 40 bilioni, kwa ajili ya ujenzi wa miundombinu ya umwagiliaji, kwenye mashamba ya uzalishaji wa mbegu ya Wakala wa Mbegu za Kilimo (ASA). Anaripoti Nasra Bakari, DMC … (endelea).

Taarifa hiyo imetolewa leo Jumatatu, tarehe 31 Mei 2021, na Naibu Waziri wa Kilimo, Hussein Bashe, akimjibu Mbunge Viti Maalum asiye na chama bungeni, Nusrat Hanje.

Katika swali lake, Hanje alihoji mpango wa Serikali katika kutumia mashamba ya uzalishaji mbegu bora, hasa zao la alizeti ili kuinua uchumi wa wananchi wa singida, wanaotegemea kilimo cha zao hilo.

Baada ya Hanje kuhoji hayo, Bashe amesema Serikali imeendelea kuweka mikakati ya kuongeza upatikanaji wa mbegu bora za mafuta nchini, kwa kutenga fedha Sh. 40 bilioni, kwa ajili ya ujenzi wa miundombinu ya umwagiliaji kwenye mashamba ASA.

“ili kuzalisha mbegu za alizeti na mbegu za mazao mengine kama vile mahindi, mpunga, michikichi, pamba, Ngano, ufuta na mazao ya bustani. Lengo ni kuondokana na utaratibu wa mkulima na wazalishaji mbegu, kwenda shamabani kwa pamoja,” amesema Bashe.

Naibu Waziri huyo wa Kilimo amesema, miundombinu hiyo ikikamilika, uzalishaji mbegu za alizeti nchini, utaongezeka kutoka tani 538.71 msimu wa 2019/20, hadi kufikia tani 10,000 (2019/30).

Bashe amesema, mbegu hizo zitatosha kutumika katika eneo la hekta 1,250,000, zinazoweza kuzalisha tani 500,000 za mafuta ya kula nchini.

“Aidha, katika kipindi cha miaka mitatu uzalishaji wa mbegu wa ASA umeendelea kuongezeka, kutoka tani 74.2 (2016/17) hadi kufikia tani 166.0 (2019/20) na sekta binafsi ilizalisha tani 372.71,” amesema Bashe.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

Watendaji Kata, Mitaa watakaoshindwa kusimamia usafi kukiona

Spread the love  WATENDAJI wa kata, mitaa na vitongoji na maofisa afya...

Habari Mchanganyiko

Mtia nia urais TLS kukata rufaa kupinga kuenguliwa

Spread the love  MTIA nia ya kugombea Urais wa Chama cha Mawakili...

Habari Mchanganyiko

NBC yazindua kampeni ya mkeka wa ushindi na ATM zake

Spread the loveBENKI ya Taifa ya Biashara (NBC) imetangaza uzinduzi wa kampeni...

Habari Mchanganyiko

Uholanzi wampongeza Rais Samia kuimarisha vyombo vya habari, demokrasia

Spread the love  UBALOZI wa Uholanzi nchini Tanzania, umempongeza Rais Samia Suluhu...

error: Content is protected !!