Friday , 29 March 2024
Home Kitengo Michezo Bil 1 za Rais Magufuli zaiweka pabaya TFF
Michezo

Bil 1 za Rais Magufuli zaiweka pabaya TFF

Walace Karia, Rais wa TFF
Spread the love

TAASISI ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa nchini (TAKUKURU), imesema inalichunguza Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF), kuhusu matumizi mabaya ya fedha, ikiwemo kiasi cha Sh. 1 bilioni kilichotolewa na Rais John Magufuli, mwaka 2019. Anaripoti Mwandishi Wetu, Dar es Salaam … (endelea).

Taarifa hiyo imetolewa leo tarehe 15 Mei 2020, jijini Dar es Salaam na Brigedia John Mbungo, Mkurugenzi wa TAKUKURU, wakati alipoulizwa kuhusu tuhuma za matumizi mabaya ya fedha, zinazolikabili shirikisho hilo.

Brigedia Mbungo ameeleza kuwa, TAKUKURU imeanza kuwahoji watu wanaohisiwa na ubadhirifu wa fedha hizo, pamoja na kukusanya nyaraka za ukusanyaji fedha na matumizi yake.

“Ni kweli Rais Magufuli alitoa fedha kwa ajili ya timu ya Taifa ya Tanzania (Taifa Stars), lakini baada ya rais kuonyesha mfano wa kuchangia, wako wadau wengine waliojitokeza kuchangia fedha. Zile fedha kweli zimetumika vibaya na taasisi inazo taarifa, imechukua hatua za kufanya uchunguzi,” amesema Brigedia Mbungo.

Wakati huo huo, Brigedia Mbungo amewataka wanaohusika na ubadhirifu huo, kurudisha fedha hizo kwa hiari.

“Tunawaita wote wanaohusika au wanahisiwa kuhusika na ugawaji au usimamiaji fedha. Tumeendelea kukusanya nyaraka za ukusanyaji fedha na matumizi yake yaliyofanyika. Huu uchunguzi unaendelea na wa kijinai. Wana hiari ya kurejesha fedha,” amesema Brigedia Mbungo.

Brigedia Mbungo amewataka wadau wa michezo, wenye taarifa juu ya ubadhirifu wa fedha katika sekta hiyo, kuipa taarifa TAKUKURU, ili izifanyie kazi kwa ajili ya kuokoa fedha za umma.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Makala & UchambuziMichezo

TFF kuamua hatima ya Amrouche

Spread the loveHATIMA ya Kocha Mkuu wa Taifa Stars, Adel Amrouche kuendelea...

Habari za SiasaMichezo

Matinyi: Dk. Ndumbaro alifanya utani ukaguzi mechi za Yanga, Simba

Spread the loveMsemaji Mkuu wa Serikali, Mobhare Matinyi amesema kauli iliyotolewa na...

Michezo

Gethsemane Group Kinondoni (GGK) waachia video ya Bwana Wastahili

Spread the loveWAIMBAJI maarufu nchini kutoka Gethsemane Group Kinondoni (GGK)SDA wameachia video...

BiasharaMichezo

Gamondi kocha bora mwezi Februari, NBC yamjaza manoti

Spread the loveBenki ya Taifa ya Biashara (NBC) ambae ni mdhamini Mkuu...

error: Content is protected !!