Monday , 11 December 2023
Home Habari Mchanganyiko Bihimba achangia ujenzi wa msikiti, awapa neno waislamu
Habari Mchanganyiko

Bihimba achangia ujenzi wa msikiti, awapa neno waislamu

Spread the love

MWANAHARAKATI huru, Bihimba Mpaya, amechangia ujenzi wa msikiti katika Madrasa ya Muhajirina, iliyoko Mtaa wa Kigezi Chini, wilayani Ilala, Jiji la Dar es Salaam, kwa kutoa matofali 1,750 pamoja na mifuko 10 ya saruji. Anaripoti Regina Mkonde, Dar es Salaam…(endelea).

Msada huo umekabidhiwa leo tarehe 17 Novemba 2023 na Bihimba kwa kiongozi wa madrasa hiyo, Ostadh Amir Mussa Mohammed, jijini Dar es Salaam.

Akizungumza baada ya kukabidhi vifaa hivyo, Bihimba, aliwataka waislamu wengine wajitokeze kuchangia ujenzi wa msikiti ili kuwezesha kazi ya uenezaji dini kwa waumini wengine.

“Nimetoa misaada mbalimbali kwa ajili ya ujenzi wa madrasa na msikiti ili kuhakikisha kazi ya Allah ya kueneza usilamu kwa waumini wake inafanyika. Waislamu wenzangu hamjachelewa toeni michango sababu msikiti lazima ujengwe,” amesema Bihimba.

Katika hatua nyingine, Bihimba amesema anawasiliana na wadau wengine, ili kuona namna ya kujenga kisima katika madrasa hiyo, kwa ajili ya upatikanaji maji.

Mwanaharakati huyo ametoa msaada huo baada ya Ostadh Mohamed kuwaomba wasilamu wachangia ujenzi wa madrasa na msikiti, ili kuondoa changamoto ya waumini kusoma pamoja na kuswali nje ya mti.

“Tunashukuru kwa msaada alioutoa Bihimba, lakini tunaomba wanaotusikiliza sasa hivi wajue bado tunahitaji msaada na madrasa yetu bado tuna ujenzi. Tulikuwa tunasoma kwenye nyumba ya makuti lakini kutokana na mvua imeharibika hivyo tunasoma kwa shida chini ya mti na mvua hii,” amesema Sheikh Mohamed.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

Amsons Group watoa milioni 100 waathirika maafa Hanang

Spread the loveKAMPUNI ya Amsons Group kupitia kampuni zake za Camel Oil...

Habari Mchanganyiko

Kesi ya mfanyakazi wa CRDB itaendelea J’tatu

Spread the love  MAHAKAMA ya Hakimu Mkazi Kinondoni, Dar es Salaam inatarajia...

Habari Mchanganyiko

Mawasiliano Dar – Bagamoyo yarejea

Spread the loveMAWASILIANO ya barabara ya Mkoa wa Pwani na Dar es...

Habari Mchanganyiko

Tanesco: Mvua chanzo kukatika umeme leo

Spread the loveShirika la Umeme Tanzania (TANESCO) limedai kuwa hitilafu iliyojitokeza katika...

error: Content is protected !!