Monday , 29 May 2023
Home Kitengo Habari Kimataifa Bobi Wine kumpinga Museven mahakamani
Kimataifa

Bobi Wine kumpinga Museven mahakamani

Robert Kyagulanyi 'Bobi Wine', akipiga kura katika Uchaguzi Mkuu wa Uganda
Spread the love

KIONGOZI wa Chama cha upinzani nchini Uganda cha National Unity Party (NUP), Robert Kyagulanyi maarufu Bobi Wine amesema, atakwenda mahakamani kupinga matokeo yaliyompa ushindi wa urais Yoweri Mseven. Inaripoti mitandao ya kimataifa … (endelea).

Bobi Wine alikuwa miongoni mwa wagombea urais katika uchaguzi mkuu uliofanyika tarehe 14 Januari 2021 ambapo, Tume ya Uchaguzi Uganda (EC), ilimtangaza Museveni kuwa mshindi kwa kupata kura 5,851,037 sawa na asilimia 58.64 ya kura zote zilizopigwa.

Bobi Wine, alishika nafasi ya pili akipata kura 3,475,398 sawa na asilimia 34.83 ya kura zote 9,978,093 ikiwa ni sawa na asilimia 57.22 ya idadi ya watu waliojiandikisha kwenye daftari la wapiga kura.

Yoweri Museveni

Kutokana na matokeo hayo, chama cha NUP kimetoa taarifa ya kwenda kupinga matokeo hayo mahakamani huku kikiwataka wanachama wao, kutokufanya fujo.

Bobi Wine alitumia ukurasa wa Twitter wa NUP kutoa ujumbe kwa wafuasi wake akisema “nachukua uamuzi huu kwa uchungu kuwasihi kujizuia kufanya aina yoyote ya fuju. Tunajiandaa kuwasilisha mahakamani malalamiko ya kupinga matokeo ya uchaguzi yaliyokuwa na kasoro za dhahiri kwa maslahi ya ushindi wa muda mrefu ujao na kwa Uganda.”

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Kimataifa

Mkutano wa Quad Hiroshima waibuka na kutafuta amani na ustawi wa Indo-Pacific

Spread the love  JITIHADA za mazungumzo ya Pande Nne (Quad), hazikuthaminiwa na...

KimataifaTangulizi

Mtuhumiwa wa mauaji ya halaiki ya Rwanda akamatwa Afrika Kusini

Spread the love  MMOJA wa watuhumiwa wakuu wa mauaji ya Kimbari ya...

Kimataifa

Kiwango cha ukosefu wa ajira nchini China chaongezeka

Spread the love  WAKATI kiwango cha ukosefu wa ajira kwa vijana nchini...

Kimataifa

Kampuni za kigeni zahofia kuendelea na biashara China

Spread the love OPERESHENI ya kiuchunguzi inayofanywa na Serikali ya China kwa...

error: Content is protected !!