Friday , 19 April 2024
Home Kitengo Habari Kimataifa Bobi Wine kumpinga Museven mahakamani
Kimataifa

Bobi Wine kumpinga Museven mahakamani

Robert Kyagulanyi 'Bobi Wine', akipiga kura katika Uchaguzi Mkuu wa Uganda
Spread the love

KIONGOZI wa Chama cha upinzani nchini Uganda cha National Unity Party (NUP), Robert Kyagulanyi maarufu Bobi Wine amesema, atakwenda mahakamani kupinga matokeo yaliyompa ushindi wa urais Yoweri Mseven. Inaripoti mitandao ya kimataifa … (endelea).

Bobi Wine alikuwa miongoni mwa wagombea urais katika uchaguzi mkuu uliofanyika tarehe 14 Januari 2021 ambapo, Tume ya Uchaguzi Uganda (EC), ilimtangaza Museveni kuwa mshindi kwa kupata kura 5,851,037 sawa na asilimia 58.64 ya kura zote zilizopigwa.

Bobi Wine, alishika nafasi ya pili akipata kura 3,475,398 sawa na asilimia 34.83 ya kura zote 9,978,093 ikiwa ni sawa na asilimia 57.22 ya idadi ya watu waliojiandikisha kwenye daftari la wapiga kura.

Yoweri Museveni

Kutokana na matokeo hayo, chama cha NUP kimetoa taarifa ya kwenda kupinga matokeo hayo mahakamani huku kikiwataka wanachama wao, kutokufanya fujo.

Bobi Wine alitumia ukurasa wa Twitter wa NUP kutoa ujumbe kwa wafuasi wake akisema “nachukua uamuzi huu kwa uchungu kuwasihi kujizuia kufanya aina yoyote ya fuju. Tunajiandaa kuwasilisha mahakamani malalamiko ya kupinga matokeo ya uchaguzi yaliyokuwa na kasoro za dhahiri kwa maslahi ya ushindi wa muda mrefu ujao na kwa Uganda.”

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

KimataifaTangulizi

Mkuu wa majeshi Kenya afariki, Ruto atangaza maombolezo

Spread the loveRais wa Kenya, William Ruto ametangaza maombezo ya siku tatu...

Kimataifa

Majaji kuamua hatima ya Zuma leo

Spread the loveMajaji nchini Afrika Kusini leo Jumanne wataamua ikiwa rais wa...

Habari za SiasaKimataifa

Spika Afrika Kusini ajiuzulu kwa tuhuma za rushwa

Spread the loveSpika wa Bunge la Afrika Kusini, Nosiviwe Mapisa-Nqakula ametangaza kujiuzulu...

Habari MchanganyikoKimataifa

Tetemeko la ardhi laua 7, lajeruhi 800 Taiwan

Spread the loveWatu wapatao saba wamefariki dunia na wengine zaidi ya 800...

error: Content is protected !!