Saturday , 10 June 2023
Home Habari Mchanganyiko Biashara ya ngono yamwibua Lugola
Habari Mchanganyiko

Biashara ya ngono yamwibua Lugola

Spread the love

WATU wanaosafirisha watoto wa kike kutoka mikoa mbalimbali ndani na nje ya nchi kwa ajili ya kufanya biashara ya ngoni, waonywa. Anaripoti Mwandishi Wetu … (endelea).

Kangi Lugola, Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi ametoa onyo hilo leo tarehe 30 Julai 2019, wakati akihutubia katika maadhimisho ya siku ya kupinga baishara haramu ya usafirishaji binadamu, yaliyofanyika jijini Dar es Salaam.

Lugola amesema, waathirika wakubwa wa biashara hiyo ni watoto wadogo wa kike wenye umri kuanzia miaka 13 hadi 24, ambapo wengi wao hutolewa maeneo ya vijijini na kuletwa mjini.

“Biashara haramu ya usafirishaji wa binadamu hapa nchini inayoongoza ni ya kutoka mkoa mmoja kwenda mwingine, waathirika ni watoto wadogo, wasichana na vijana ambao wako katika umri wa miaka 13 hadi 24,” amesema Lugola.

Lugola amesema, Jiji la Dar es Salaam linaongoza kwa biashara haramu ya usafirishaji binadamu, likifuatiwa na Tanga na Dodoma.                                                     

“Watu wanasafirishwa nje kwa kuahidiwa kazi nzuri, wengi wanatokea la Dar es Salaam, Tanga na Dodoma, waathirika ni wanawake wenye miaka 16 – 26, ingekuwa ni kuku umri huu tungewaita mtetea kwa sababu wakifika kule wanafanya biashara ya ukahaba,” amesema Lugola.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

Askari Polisi zaidi ya 100 wapigwa msasa wa udereva kukabiliana na ajali

Spread the love  KATIKA kuhakikisha wimbi la ajali za barabarani zinapungua kama...

Habari MchanganyikoTangulizi

Serikali yakana kuhamisha kwa nguvu jamii ya Kimasai Loliondo

Spread the loveWAZIRI wa Katiba na Sheria nchini Tanzania, Dk. Damas Ndumbaro,...

Habari Mchanganyiko

Tunduma watenga 60 milioni kujenga machinjio ya kisasa

Spread the loveHALMASHAURI ya mji Tunduma Imetenga kiasi cha Tshs Miloni 60...

Habari Mchanganyiko

Bilioni 17 kujenga bandari kavu Tunduma

Spread the loveHALMASHAURI ya mji Tunduma iliyopo wilayani  Momba mkoani Songwe imepatiwa...

error: Content is protected !!